Advertisements

Monday, July 28, 2014

UCHAGUZI DMV, MASWALI MEPESI

Ndugu wana DMV wenzangu , uongozi Bora ni ule utakaoweza kuiweka jumuia yetu sehemu bora na Kuiwekea heshima kama ilivyofanywa kazi hiyo na Uongozi wa Kaka Iddi Sandaly. Kwa kifupi wote tunajuwa sera za  uongozi huu wa Mhe. Iddi zinaongozwa na sera yake ya kwanza ambayo ni umoja kwa watanzania wote.

Nimesikiliza Video ya Mhe. Libe, nimestuliwa kwa kusikia kwamba anakubali kuwa Jumuia yetu ni Non-Profit kwa maana ni chombo ambacho si cha kibiashara. Lakini anaeleza kwamba kwenye uongozi wake kuwa Jumuia itatoa mikopo kwa watanzania au wafanya biashara wadogo wadogo. Non- profit hairuhusiwi kutoa mikopo hata biashara ya kawaida hairuhusiwi kutoa mikopo (Loans).

Mikopo inatolewa na Financial institution (banks). Sasa hii sera imekaaje wana  DMV?. Ushauri wangu mimi naomba wagombea watupe sera ambazo ni za kweli kuliko kusema vitu ambavyo havina ukweli au ufafanuzi. 

Mchango wangu wa pili ni kuhusu Mhe. Libe alipogusia kuwa ataanzisha Nurse Association ya watanzania. Kwenye hili naona mitafaruku miwili apa ambayo nadhani mimi kama mpiga kura nadhani inaashiria kuwa hili lina longolongo.

Kwanza, Jumuia kama Association haiwezi kuanzisha Association nyingine ndani yake. Nikiwa na maana kwa sheria ya nchi hii Non- profit haiwezi kuwa na non- profit nyingine ndani yake.

Pili. Je Kwanini tuangalie Nurses tu?. Najuwa hii ni professional ya Mhe. Libe, lakini hapa DMV kuna watu  ambao wanafanya kazi za aina mbali mbali. Sidhani kama ni sahihi kuwasahau watu wa nyanja nyingine. Nadhani uongozi bora ni lazima uhakikishe unawapa watu wote haki sawa, kuna mafundi magari, madereva, ma bloggers ,  nk.

Najuwa uongozi unaomaliza muda wake ukiongozwa na Rais na Mgombea wa muhula wa pili Mhe. Sandaly, uliunda kamati ya Social and economic Empowerement. ambayo imekuwa ikitupa matangazo ya Kazi, Mafunzo na mengineyo. Nadhani isingekuwa sahihi kaka Sandaly kama angesema anaanzisha Tanzanian Accountants Association , kwa vile yeye Sandaly ni Accountant.

Naomba kaka Libe awe anatupa sera  zenye kuweza kutolewa kwenye mabano.

Faustus


2 comments:

Anonymous said...

Muuliza maswali anaonekana ni mtu wa majungu na upeo wa kufiri na sawa na urefu wa maswali yake. Mdau nje ya Marekani

Anonymous said...

Waana DMV, tuweni makini tusije UUWA huu Muungano. Sisi kama sisi tunatakiwa kujiendeleza wenyewe kwa kila aina ya michango na sio kutegemea bure au vyama kuanzishwa ndani ya vyama!!sisi wenyewe ndio nguzo ya huu umoja. Asanteni.