Advertisements

Thursday, July 31, 2014

UZINDUZI WA TOVUTI YA MABADILIKO YA TABIANCHI

Uzinduzi wa tovuti ya Mabadiliko ya Tabianchi pamoja na mkataba wamkataba wa uwanzishwaji wa kituo cha Taifa cha kukusanya na kuratibu takwimu za hewa ukaa
 Sehemu ya waandishi wa habari waliyoudhulia katika uzinduzi huo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira Mh. Dkt. Eng Binilith Satano Mahenge akizindua rasmi tovuti ya mabadiliko ya tabianchi itakayotumika kutoa taarifa mbalimbali za utunzaji wa Mazingira.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira Mh. Dkt. Eng Binilith Satano Mahenge (wa kwanza kushoto) akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) katika ukumbi wa mkutano wa  Ofisi ya Makamu wa Rais leo jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa "tovuti ya mabadiliko ya tabianchi" huku akieleza malengo ya tovuti hiyo. kushoto ni Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Julius Ningu.
 sehemu ya wadau waliyoudhulia katika mkutano huo kushuhudia makubaliano ya mkataba huo.
 Mkuu Msaidizi wa Chuo cha kilimo SUA Prof. Gerald Monella (aliyesimama) akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wadau mbalimbali kuhusu mkataba huo unaofanyika baina ya Ofisi ya Makamu wa Rais na chuo cha SUA.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Sazi Salula (wa kwanza kushoto) na Mkuu Msaidizi wa Chuo cha SUA Prof. Gerald Monella wakisaini mkataba wa uwanzishwaji wa kituo cha Taifa cha kukusanya na kuratibu takwimu za hewa ukaa  uliofanyika katika ukumbi wa mkutano Ofisi ya Makamu wa Rais jijini Dar es Salaam.
 Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Sazi Salula wakipeana Mkataba na mkuu msaidizi wa wa chuo cha kilimo SUA Prof. Gerald Monella baada ya kusaini.

Mheshimiwa Eng Dkt. Binirithi S. Mahenge (mbunge) Waziri wa nchi ofisi ya Makamu wa Rais (mazingira) azindua tovuti ya mabadiliko ya tabia nchi.

Katika hotuba yake fupi ya uzinduzi wa tovuti hiyo, aliyoandaliwa kwa ufadhili wa serikali ya Denmark Mh. Binirithi Mhenge amesema kuwa mabadiliko ya tabia ya nchi huangaliwa kwa muda wa miaka 30 hivyo kwa kipindi hiki chote kumekuwa na madhara mengi yatokanayo na athari za mabadiliko ya tabia Nchi ikiwa ongezeko la joto, kina cha bahari kuongezeka pamoja na ongezeko la majanga ya mvua zisizo na viwango, kutoka na shughuli za binadamu katika uzalishaji hasa viwanda vikubwa

Alisema kwa tovuti inayozinduliwa ina umuhimu mkubwa kwani inaelezea maeneo ya hali ya mabadiliko ya tabia nchi na juhudi za serikali katika kukabiliana na athari zinazoletwa na mabadiliko hayo.

“ziko sababu za kuungana na wenzetu ili kuondoa tatizo hili la mabadiliko ya nchi ambapo tovuti hiiWWW.climatechange.go.tz inatuunganisha na tovuti mbali mbali katika kupunguza gesi joto hapanchini pia inaelezea fursa zilizopo katika miradi na program mbali mbali. Alisisitiza”

Alibaini kuwa tovuti hii itachangia kwa kiasi kikubwa kuongeza uelewa na weledi kuhusu mabadiliko ya tabia nchi nchini kwa wananchi na wadau kwa ujumla.

No comments: