Advertisements

Monday, July 7, 2014

WANAWAKE WATOROKA BOKO HARAM


Zaidi ya wanawake na wasichana 60 wameripotowa kutoroka kutoka katika kundi la Boko Haram, kwa mujibu wa vyanzo vya kiusalama.
Wanawake na wasichana hao ni
miongoni mwa 68 waliotekwa mwezi uliopita karibu na mji wa Damboa, kaskazini mashariki mwa jimbo la Borno.
Taarifa zinasema wanawake hao walitoroka wakati wapiganaji walipokwenda kuvamia kambi moja ya jeshi karibu na Damboa siku ya Ijumaa.
Jeshi la Nigeria limesema liliwaua zaidi ya waasi 50 katika mapigano.
Boko Haram bado inawashikilia zaidi ya mabinti 200- wanafunzi waliotekwa mwezi Aprili.
Katika picha ni kiongozi wa Boko Haram, Abubakar Shekau.

No comments: