Advertisements

Saturday, July 12, 2014

ZIARA YA NAIBU MAWAZIRI NISHATI NA MADINI, MAZINGIRA, TAMISEMI NA WABUNGE NCHINI CANADA

Ujumbe wa Tanzania uliopo nchini Canada kwa ziara ya mafunzo ukiongozwa na Naibu Waziri Nishati na Madini, Charles Kitwanga (aliyenyoosha mkono), ukiwa katika chumba cha kusimamia mitambo ya kuzalisha methano (haionekani pichani) katika kiwanda cha kuzalisha malighafi hiyo kilicho katika jimbo la Alberta nchini Canada.
Ujumbe wa Tanzania uliopo nchini Canada ukiongozwa na Naibu Waziri Nishati na Madini, Charles Kitwanga (wa nne kutoka kushoto, waliosimama), ukiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa kampuni ya kimataifa ya kuzalisha na kusafirisha methano ya nchini Canada mara baada ya kufanya ziara ya mafunzo katika kiwanda hicho. Wengine katika picha ni Naibu Waziri, TAMISEMI, Kassim Majaliwa, (wa nne kutoka kulia, waliosimama). Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira, Ummy Mwalimu, (wa pili kutoka kulia waliosimama) pamoja na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini na wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini. 

Father Kidevu

No comments: