Advertisements

Friday, August 1, 2014

RAIS WA ZANZIBAR DKT. ALI MOHAMED SHEIN AFUNGUA RASMI MAONESHO YA NANE NANE, 2014 KITAIFA, MKOANI LINDI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Ali Mohamed Shein(kulia) akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Mkoa wa Lindi Mhe. Agnes Hokororo mapema leo Agosti 1, 2014 alipowasili Viwanja vya Gongo tayari kwa ufunguzi rasmi wa Maonesho ya 21 ya Wakulima na Wafugaji yanayofanyika Mkoani Lindi Kitafa kwa mara ya kwanza tangu yaanzishwe hapa Nchini.
Waziri wa Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi, Mhe. Dkt. Titus Kamani akitoa Salaam za Wizara katika Maonesho ya Nane Nane Kitaifa kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi, Rais wa Zanzibar Alhaj Dkt. Ali Mohamed Shein(Meza Kuu)katika ufunguzi wa Maonesho hayo ya Wakulima na Wafugaji ambayo yanafanyika Mkoani Lindi Kitaifa.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Ali Mohamed Shein(katika Jukwaa) akiwahutubia Wakulima, Wafugaji pamoja na Wananchi wa Mikoa ya Kusini yaani Lindi na Mtwara katika Ufunguzi rasmi wa Maonesho ya Nane Nane Kitaifa yanayofanyika katika Viwanja vya Gongo, Mkoani Lindi leo Agosti 1, 2014.
Baadhi ya Washiriki mbalimbali wa Maonesho ya Nane Nane Kitaifa wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi Rais wa Zanzibar, Alhaj Dkt. Ali Mohamed Shein(hayupo pichani). Waliovaa Tisheti za Bluu ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza toka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza Kitengo cha Kilimo na Mifugo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Ali Mohamed Shein akipata maelezo toka kwa Maafisa Wataalamu wa Benki Kuu ya Tanzania ya namna Wakulima wanavyoweza kupata dhamna ya Mikopo katika Mabenki mbalimbali hapa Nchini kwa Benki Kuu ya Tanzania alipotembelea Banda hilo leo Agosti 1, 2014 katika Sherehe za Maonesho ya Nane Nane Kitaifa yanayofanyika Mkoani Lindi kwa mara ya kwanza.
Wasanii wa Kikundi cha Utamaduni wakicheza ngoma ya kijadi Maarufu sana Mkoani Lindi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Ali Mohamed Shein akiondoka katika Viwanja vya Gongo vya Maonesho ya Nane Nane Kitaifa mara tu baada ya kukamilisha shughuli ya uzinduzi huo leo Agosti 1, 2014 Mkoani Lindi(Picha zote na Lucas Mboje).

No comments: