Advertisements

Friday, September 19, 2014

TASWIRA,MWIGULU NCHEMBA ANAISHI HIVI NA WANANCHI WAKE KAMA KUMBI KUMBI

Comrade Mwigulu Nchemba akiwa amembeba Mtoto katika kijiji cha kaselya wakati alipotembelea kukagua Usambazaji wa Nguzo za Umeme na Waya Jimboni Iramba.
 Mh,Mwigulu Nchemba akiteta jambo na Mama huyu Mlemavu wa Ngozi ambaye Mwigulu amekuwa akimsaidia katika Maisha yake,Hapa Mama huyu amebarikiwa kupata mtoto hivyo anamuonesha Mbunge wake hapa Iramba,Comrade Mwigulu Nchemba akimsikiliza Mwananchi wake mwenye Ulemavu katika kijiji cha Ndulungu Jimboni Iramba.Mh.Mwigulu Nchemba akipokea zawadi ya Kibao kilichonakishiwa kwa maneno "MH:MWIGULU MKOMBOZI WA IRAMBA|".Hakika kwa sasa Jimbo la Iramba limefanikiwa kupata miradi ya maendeleo mingi ikiwamo Umeme,Barabara,Hospitali na shule kwa kiwango kikubwa hazijawahi kuwepo Iramba,Hivyo juhudi za Mbunge zimepelekea Iramba sasa kusambazwa Umeme Vijiji vyote.

Mmoja ya Wanafunzi ambao Mwigulu amepata kuzungumza naye kuhusu masomo na hali ya shule,Mwigulu anasomesha watoto waliokatika mazingira magumu zaidi ya 300 jimboni kwake,Wengine wameshahitimu kidato cha sita.
Vijana wakiteta na Mbunge wao kuhusu Vifaa vya Michezo.Comrade Mwigulu Nchemba akisikiliza kwa makini tatizo la huyu mama na mtoto wake katika kijiji cha Ndulungu Jimboni Iramba.

Hii ni sehemu tu ya Furaha ya Wananchi wanapokutana na Mbunge wao ambaye amewaletea maendeleo hapa Iramba ambayo yalikuwa ni ndoto kwao,Ujenzi wa shule,Maabara,Umeme,Zahanati kila kata,Barabara nk
Picha/Maelezo na Sanga Jr.

No comments: