Askari Polisi wakiwapakia baadhi ya Wafanyabiashara ndogo ndogo(MMACHINGA) walioleta vurugu maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam leo.
Mkazi wa jiji akisaidiwa na wasamalia wema baada ya kuzimia kutokana na kupatwa na mstuko baada ya Polisi kupiga Mabomu katika sakata hilo.
Mkazi wa jiji akisaidiwa na wasamalia wema baada ya kuzimia kutokana na kupatwa na mstuko baada ya Polisi kupiga Mabomu katika sakata hilo.
Baadhi ya Mashuhuda wakisaidia Mkazi huyo kuhakikisha anapelekwa katika kupata Huduma ya kwanza.
Msamaria akiwa na Mkazi huyo wa jijini baada ya purukushani za Machinga dhidi ya Polisi jijini Dar es Salaam leo.
JESHI la Polisi jijini Dar limelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafanyabiashara ndogondogo maarufu kwa jina la Machinga waliokuwa wanaandamana kuelekea ofisi za jiji eneo la Kamata, Kariakoo jijini Dar es Salaam leo.
Machinga hao waliamua kuchoma matairi na kuweka mawe barabarani wakati wa maandamano hayo ambapo madai yao ni kuhusu unyanyasaji wanaofanyiwa na askari wa jiji ikiwemo kunyang'anywa mali zao.
(PICHA NA MAKONGORO OGING' / GPL)




No comments:
Post a Comment