Advertisements

Monday, January 26, 2015

ACT Walia Kiongozi wao Kuuawa......Ni yule Aliyechinjwa Kinyama na Kupikwa kwenye Sufuria kama Nyama ya Kuku

CHAMA cha ACT-Tanzania kimelitaka Jeshi la Polisi nchini kuwasaka na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wote waliohusika na tukio la mauaji ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kitongoji cha Masigo wilayani Mlele mkoani Katavi, Christian Kahongo.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Katibu Mkuu wa ACT-Tanzania, Samson Mwigamba, ilieleza kuwa chama hicho kinalaani mauaji hayo ya kinyama ambayo hayaendani na haki za binadamu.
Alisema walimkata kichwa na kukitenganisha kabisa na kiwiliwili kisha wakakata sehemu za siri na baadhi ya viungo vingine vya kichwa wakaanza kuvikaanga kwenye sufuria.
Alisema huo ulikuwa ni unyama wa ajabu ambao hatujawahi kuushuhudia.
“ACT-Tanzania tumepoteza shujaa namba moja kati ya mashujaa wanaokiwakilisha chama chetu kwenye vyombo vya Serikali. Ndiye mshindi wa kwanza kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kupitia ACT-Tanzania na alipita bila kupingwa na kuwa wa kwanza kutangazwa kuwa Mwenyekiti wa Kitongoji cha Masigo kupitia ACT-Tanzania.
“Tumepoteza shujaa kama chama taifa, Mkoa wa Katavi umepoteza shujaa, Jimbo la Mlele wamepoteza shujaa, vivyo hivyo kwa wanachama wa Kata ya Inyonga na tawi la Inyonga,” alisema Mwigamba.
Alisema chama kitashiriki msiba huo kwa kuwakilishwa na Mwenyekiti Taifa wa muda pamoja na Katibu wa Ngome ya Vijana Taifa.
“Ikumbukwe kuwa wauaji hawana rangi, kabila wala vyama, pia hawachagui nani wa kumuua kama ilivyotokea hivi karibuni kwa askari wetu katika Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani.
“Sisi ACT-Tanzania tunalaani kwa nguvu zote mauaji haya ya kiongozi wetu si tu kwa sababu aliyeuawa ni kiongozi wa ACT-Tanzania, bali tutalaani na kupinga mauaji ya Mtanzania yeyote,” alisema Mwigamba.
Tukio hilo la mauaji ya kinyama lilitokea Januari 24, mwaka huu ambapo watu wasiojulikana walivamia nyumbani kwa Christian Kahongo na kumuua kwa kumkatakata mapanga.
Picha za Mwenyekiti wa Kitongoji aliyechinjwa na kupikwa ndani ya Sufuria
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Songambele, Kata ya Ilela Tarafa Inyonga Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi, Richard Madirisha (31), ameuawa kikatili kwa kuchinjwa shingo na kutenganishwa na kiwiliwili na kisha kunyofolewa viungo vya mikono na miguu na sehemu za siri na kichwa chake na viungo hivyo kupikwa ndani ya safuria kama mboga.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari mauaji hayo ya kikatili na kutisha yalitokea juzi saa 5.30 usiku nyumbani kwa marehemu.
Kidavashari alisema, siku hiyo ya tukio marehemu alikuwa amelala nyumbani kwake akiwa na mkewe Meklina Mussa na ghafla walitokea watu watano ambao hawafahamiki na kuvunja mlango na kuingia ndani ya nyumba.
Alisema watu hao waliodaiwa kuwa na mapanga waliingia chumbani kwa marehemu na kumlazisha mkewe ajifiche kwa kujifunika na shuka usoni.
Alisema baada ya mkewe kujifunika walianza kumchinja marehemu kwa kutumia panga huku mkewe akiwa anasikia jinsi marehemu akilia kwa uchungu.
Kidavashari alisema baada ya kumchinja walichukua kichwa na kukiweka kwenye safuria na maji na kukipika kwenye moto uliokuwa unawaka nje ya nyumba ya marehemu.
Alisema kisha walirudi ndani na kunyofoa sehemu za siri, mikono na miguu na kuziweka kwenye safuria jingine kwenye moto na kutokomea kusikojulikana huku viungo hivyo vikiendelea kuchemka ndani ya safuria hizo.

No comments: