Advertisements

Wednesday, February 4, 2015

MATAYARISHO YA UJIO WA RAIS WA SHIRIKISHO LA UJERUMANI ZANZIBAR

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akitembelea Bandari ya Malindi kuangalia matayarisho ya ujio wa Rais wa shirikisho la Ujerumani Bwana Joachik Gauck.

Kushoto ya Balozi Seif ni Mshauri wa Rais anaesimamia Uchumi, Uwekezaji na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Moh’d Ramia na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari Zanzibar Nd. Abdulla Juma Abdulla.
Balozi Seif akiwa na Viongozi wa Kamati ya kuratibu Mapokezi ya Rais wa Ujerumani wakirudi kukagua eneo la kushukia boti ziendazo kwa kasi katika Bandari ya Malindi.

Kushoto yake ni Mshauri wa Rais Balozi Moh’d Ramia, Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar Balozi Silima Kombo Haji pamoja na Mkurugenzi Bandari Nd. Abdulla Juma.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiwa pamoja na Balozi Mdogo wa Heshima wa Shirikisho la Ujerumani hapa Zanzibar Balozi Has –Dieter Allgaier wakielekea kukagua chum,baa cha watu Mashuhuri { VIP } kiliopo Bandari ya Malindi ambacho kimewekwa hakiba kwa ujio wa Rais wa Shirikisho la Ujerumani Bwana Joachim Gauck.
Mshauri wa Rais anayesimamia Uchumi,Uwekezaji na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Moh’ d Ramia akimuelezea Balozi Seif hatua zilizochukuliwa katika matayarisho ya ujio wa Rais wa Ujerumani.

Kati kati yao ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Moh’d Aboud Moh’d na kulia ya Balozi Ramia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar Balozi Silima Kombo Haji.

Picha na – OMPR – ZNZ.

No comments: