ANGALIA LIVE NEWS

Monday, March 23, 2015

WATANZANIA LAZIMA TUWE MAKINI NA MATAJIRI WA NCHI HII KWA MUSTAKABALI WA TAIFA LETU NA USTAWI WA WATANZANIA MASKINI

Ni wazi kwamba ningependa siku moja watanzania waweze kujua ukweli wa nini kinafanywa na matajiri wa nchi hii.Matajiri waliojaa  ulafi wa kunufaika na rasilimali za nchi hii kwa manufaa yao na familia zao ukijumlisha wapambe wao na washirika wa ndani na nje ya nchi hii ya Tanzania. Ni katika vita hii ndio inayopelekea serekali yetu kuyumba na kuyumbishwa (STATE TO BE CAPTURED) na hawa matajiri pale wanapopigania maslahi yao na kudiriki kutumia utajiri wao na umiliki wao wa vyombo kama vya Habari wanavyomiliki ili kuongeza kasi ya mapambano hayo ya kudai maslahi yao . Ni kweli kabisa kwamba hawa matajiri wamejipanga kikamilifu na kujipanga kwao kupo katika Nyanja tofauti sana lakini Nyanja zote wanazotumia huwa wako makini sana na hivyo pia wanahitaji wananchi na serekali makini kuweza kupambana na mipango yao hiyo michafu iliyogubikwa na hulka ya ulafi na ubinafsi wa hali ya juu.Mipango hii ya matajiri katika kupambana kuhakikisha wanapata maslahi yao inaanzia kwenye kutumia vyombo vya Habari wanayomiliki wao wenyewe au washirika wao au zaidi ni vile wanavyovinunua ili viweze kupeperusha ,kutetea na kuandika maslahi yao.Katika kufanya kwao hivi huwa wanatumia vyombo vya Habari hivi kujaribu na kuhakikisha kwamba wanaaminisha watanzania kwamba serekali inania ya kuwanyima kile wanachoomba na kupendelewa watu wa nje au mashirika ya kiserekali. Wakiwa wanafanya hivyo pia hujumuisha Habari na uzushi unaokuwa umelenga kutaka kupata huruma ya watanzania kwamba hawa walafi waliojipa jina la wazawa wanaonewa na hivyo watanzania wapaze sauti zao kuwatetea kwani watakapo pata kuvuna hizo rasilimali manufaa yatakuwa kwa taifa lote .Loooo huu ndio uzandiki na unafiki ambao wanawavika watanzania na kuwaaminisha na hii huwafanya kuwaaminisha kwamba maslahi yao binafsi wanayopigania ni lazima watanzania wote washiriki kuyapigania kwani ni maslahi ya taifa .Kumbe huu ni uuongo wa mchana kweupe kabisa wa kusema maslahi yao yakitimia taifa nalo kwa ujumla litafaidika na hii hupelekea watanzania kuanza kuwaona hawa matajiri kama watetezi wao kumbe maskini watanzania hawajui kwamba ni bora shirika la serekali likahodhi uvunaji wa rasilimali manufaa yatakuwa ya uma na sio kama wanavyoaminishwa na matajiri walafi . Matajiri wanotumia vyombo vya habari vyao kugeuza maslahi yao kuwa maslahi ya taifa.


Hii ndio hatari ya nchi yetu ilipofikia kwa hawa matajiri wa nchi hii kujivika ngozi ya kondoo kumbe maskini wao ni chui . Nimependa sana kuielezea hali hii nikuusisha na sakata la ugawaji wa vitalu vya gesi katika nchi yetu.Ni wazi kwamba katika mchakato mzima wa kuomba vitalu hivyo vya gesi katika maeneo ambayo gesi imegunduliwa katika mkoa wa Mtwara, tuliano mashambulizi mengi ya hoja zilizokuwa zikiibuliwa na matajiri katika nchi hii wakitaka serekali iweze kuwapa upendeleo. Ni katika vita hii ya kutaka kupendelewa na serekali kwa wawekezaji wa ndani ndio iliyoweza kuibua mjadala mrefu ,mjadala ulivikwa sifa ya kitaifa kumbe ulikuwa mjadala uliibuliwa na matajiri wachache waliokuwa wakipigania maslahi yao lakini kwa ustadi wao na utajiri wao wakaoufanya uwe ni mjadala wa kitaifa. Looo tukaona watanzania wanyonge wakilalamika kwamba jamani mnaona serekali hii inawanyima wazawa fursa ya kuchimba gesi na inawapendelea wageni .Huu ndio ulikuwa mwazo wa malumbano kati ya serekali na watanzania matajiri na walalaahoi waliokuwa wamejazwa fikira potofu kwamba watanzania matajiri wanabaguliwa na serekali hali yakuwa wanauwezo.Nakumbuka hili jambo lilizuwa mjadala mrefu sana na midahalo mingi iliyokuwa imesheheni kwenye majumba ,mashule ,maskani ya watanzania na hata kwenye ofisi na taasisi mbalimbali .Ni kweli kwamba matajiri hawa waliokuwa na maslahi yao binafsi waliweza kufanikiwa kuandaa safari hii ya mapambano kuona kwamba rasimali iliyogunduliwa ya gesi inachangia katika kuongeza utajiri wao . Kutokana na nia yao hii na uchu wao huo wa Kukuza pato lao lisilokuwa na mahusiano yeyote ya kunyanyua hali ya maisha ya mtanzania wa kawaida aliyoko kijijini anapambana na jembe la mkono alime kulilisha taifa hii na familia yake . Kujipanga huko kwa matajiri kulianza kupanga safu ya waandishi wataokuwa wakiandika Habari hizo za mapambano juu ya kufaidi hii rasimali iliyogunduliwa na kupanga safu hata ya viongozi wa umma hususani wabunge kuweza kuwatetea na kuwasemea. Mbali zaidi naweza kuongezea kwamba hii pia ilisaidwa na vyeo vyao walivyonavyo katika taasisi ya Sekta Binafsi inayotetea maslahi ya tabaka tajiri bila ya kuangalia maslahi ya kitaifa na maslahi ya mtanzania mnyonge au mlalahoi.

Hii ndio ilikuwa pata shika nguo kuchanika katika taifa hili matajiri wakiamini kwamba hapa bora punda afe mzigo ufike .Hii ni kiwa na maana kwamba ata watu wakichukia serekali yao au amani ya nchi ikivurugika sawa lakini wao lazima wahakikishe kwamba wanapata maslahi yao wanayopigania kwa kutumia pesa zao nyingi na muda,ujuzi wao mwingi. Nakumbuka wazi kwamba mjadala huu wa matajiri kutaka kupata upendeleo wa pekee kutoka serekalini utakaowafanya wao kuvuna rasilimali hii ya nchi na kutajirika kutokana na unyeti na umuhimu wa rasilimali hii ya gesi duniani na katika taifa letu hili. Uchu huu ndio uliopelekea kuandikwa kwa taarifa za upotoshaji katika vyombo vya Habari kama magazeti, mitandaoni na kutangazwa kwenye maredio na Televisheni. Taarifa zilizokuwa zimejaa chuki na maneno ya kebehi kwa viongozi wa serekali na mashirika ya serekali na serekali kwa ujumla.Yote haya yalikuwa hayafanywi kwa bahati mbaya ila  makusudi na yalifanywa hivi ili kuona ni jinsi gani serekali itaweza kutishika na harakati hizi za matajiri za kutaka maslahi yao yazingatiwe na yalindwe kwa njia yeyote ile. Ukweli ni kwamba serekeli kwa ujumla ilitetereka nadiriki kusema ila jambo la msingi ni kwamba mungu alitubariki sana kwa kutupatia kiongozi shupavu katika serekali hususani katika sekta hii ya madini  na nishati naye si mwingine bali ni Profesa Sospeter Muhongo .

Ni wazi kwamba Profesa Sospeter Muhongo ndio kiongozi wa serekali aliyekuwa akinyanyua mdomo wake mara kwa mara kupambana kwa dhati kabisa na hawa matajri waliokuwa wanajaribu kutumia vyombo vya Habari na wabunge kupigania maslahi yao,familia zao na washirika wao wa ndani na nje huku wakiwa wamejivika sura na maneno ya kizalendo. Ukweli ni kwamba vita hivi vilikuwa vikali sana kusema kweli kwasababu ni mtu mmoja ambaye alikuwa anapambana kizalendo na jopo la mawakala wa rasilimali zetu na watanzania waliopotoshwa kuhusu uvunwaji wa rasilimali ya gesi na hawa matajiri kupitia vyombo vya Habari vyao na walivyovinunua pamoja na viongozi wa uma kama baadhi ya wabunge . Nakumbuka mapambano haya ya matajiri wa ndani na mawakala wao yalifanyika huku yakiwa yanajaribu kupandikiza chuki kwa watanzania kwa serekali yao na waziri wao aliyekuwa amejaa  hoja na uchambuzi wa kizalendo . Hoja na uchambuzi wa maswala ya gesi uliokuwa umejaa uzalendo, uwazi, uwajibikaji, utaalamu na uhalisia wa mambo yenyewe yanavyotaka na ulivyo. Wapi bwana matajri walikuwa na kasi ya ajabu na maneno ya dhihaki na kebehi huku yakiwa sambamba na hoja za kishabiki Mfano “Palizushwa maneno kwamba waziri amesema mitaji ya matajiri ya watanzania ni ya kuwekeza kwenye viwanda kama   juisi tu ”. Haya yote yalikuwa ni mapambano ya kuhakikisha kwamba matajiri wanapata maslahi yao waliojitoa kwa hali na mali kuyapigania na wakiwa na imani na msimamo kwamba lolote na liwe ila chetu kwanza taifa baadae. Mbali zaidi kwa lugha za mitaani vijana wanasema “KAMA MBWAI MBWAI” .

Jambo pekee ambalo naishukuru sana taasisi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni pale ilipoona kwamba kuna haja ya huu mjadala ukaja kujadiliwa katika ukumbi wa chuo ukumbi wa Nkurumah. Huu ni ukumbi wenye sifa ya kitaaluma ya kusheheni mijadala ya kitaifa inayosukumwa na utaalamu, uzalendo na ukweli. Ni wazi kwamba jambo hili lilikuwa jema sana kwani iliweza kutoa fursa kwa matajiri na upande wa serekali kutoa hoja zao na kuchambuliwa vizuri na wasomi watanzania na watanzania wote kuona na kusikia na kuwezesha kuchambua ili kuweza kupata muafaka .Nashukuru sana katika siku ile kwa upande matajiri waliosimama kutetea upande wa matajiri waliojiita wazawa huku mimi nasema matajiri wazawa wanaopigania maslahi yao ila wakajifanya wanapigania maslahi ya taifa waliwakilishwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi  Dr. Regenald Mengi. Ni vema sana mana kwa upande wa serekali uliwakilishwa na Waziri Mtaalamu wa Jiolojia,Profesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam  Profesa Sospeter Muhongo  ambaye kusema kweli kwake ilikuwa yuko uwanja wa nyumbani waswahili wansema. Katika hali nzuri mjadala uligubikwa na hoja zlizokuwa  zimesheheni utetezi wa maslahi ila maslahi tofauti.Lakini nipende kusema jambo moja ambalo sikufurahishwa kabisa na kweli hii ilionesha kwamba matajiri wa nchi wanapigania maslahi yao na sio maslahi ya taifa ni pale Mwenyekiti wa Sekta Binafsi Tanzania Dr.Reginald Mengi pale alipotuambia watanzania na serekeali kwamba katika kuhakikisha kwamba watanzania wanafaidika na rasilimali za nchi yao na wanamiliki rasimali hizo na wanashiriki kikamilifu kuzivuna ili kuepuka laana ya rasilimali . Alituasa na kusisitiza tuige mifano ya Nchi ya Nigeria na Angola nchi ambazo uvunaji wake wa rasilimali unavunwa na matajiri wazawa. Lakini huu ulikuwa mfano wa kusikitisha kabisa na waajabu ambao ulikuwa haupaswi kutolewa na Mwenyekiti huyu tena ambaye ni Daktari kwa Elimu yake ikiwa na maana kwamba amemaliza Shahada ya Tatu .Kusema kwangu kwamba ushauri wake ni waajabu na sio sahihi hii ilithibitishwa na hoja zilizotolewa na waziri Profesa Sospeter Muhongo, msomi aliyethibitisha utaalamu wake pale alipotoa hoja nzito ambayo ni ya kweli naomba ni yaeleze kwa kuyasherehesha.
“Mwenyekiti wa TPSF anatwambia watanzania na serekali yetu tuige mifano ya Nigeria na Angola kwenye kumilikisha na kushirikisha wananchi wake (wazawa) kwenye uvunaji wa rasilamili za nchi kwa manufaa lakini kwanini ametoa mifano ya nchi ambazo zinanuka rushwa kwenye dunia ,na nikila mtu anajua kwamba nchi hizi zinanuka rushwa na hii inadhihirika katika uvunaji wa rasimali zao kama mafuta .Mfano ANGOLA  anayevuna rasimali ya mafuta na kuuza kwa manufaa yao ni Rais Do Santos na mwanaye wa kike mwanamke tajiri Afrika .Tukienda Nigeria ni familia za watu wachache wanaofaidika na uvunaji wa mafuta .Ni wazi kwamba hatuwezi kuiga nchi hizi ambazo zinanuka rushwa na nchi ambazo wananchi wake hawajafaidika na rasimali hizo .Ni wazi kwamba kama watanzania tutaiga kwenye nchi hizo itakuwa ni maafa makubwa kwenye nchi yetu na balaa kubwa ”
Hii ndio ilikuwa hoja ya dhahiri kabisa iliyoonyesha kwamba hawa matajiri hawa katika swala hili la kutaka fursa ya uvunaji wa rasilimali ya gesi katika nchi yetu ilikuwa ni mapambano yalikuwa yamegubikwa maslahi binafsi ili ya yakavikwa ngozi ya uzalendo. Yote haya yalifanyika wakijua kwamba matajiri watapata huruma ya watanzania wanyonge kuwatetea wakiamini kwamba watanzania watawaona kama watetezi wao kumbe ndio wadidimizaji kuliko serekali. Uthibitisho wa hilo ndio mana Mwenyekiti wa sekta binafsi alidiriki kutuambia kwamba tuige nchi za Nigeria na Angola ambazo zinanuka rushwa na ni matajiri ,familia zao na vibaraka wao wa ndani na nje ndio wanaofaidika na uvunaji na biashara ya mafuta na kuwaacha wananchi walalahoi katika lindi kubwa la umasikini na maisha magumu . Hii ikienda sambamba na wao kula na kusaza na kufanya birthday party za wake zao kwa kuwaita wasanii maarufu kama diamond Platinum ambaye amemlipa hela ambayo angetumia kuwagaia watanzania walioshindwa kuwa na miatano ya kununua dawa au hawajala au kufanya jambo lolote kwa watanzania maskini ,Umaskini unatokna na utajiri wao hawa matajiri wanyonyaji wa wanyonge.

Kwa nyongeza niliguswa pia na hoja ya msingi na Waziri Profesa Sospeter Muhongo kwamba huyu Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi ni miongozi mwa watanzania wanaomiliki migodi katika nchi hii ambayo wengi wao hawalipi kodi katika nchi hii.Zaidi ya hapo ni kwamba anamiliki hekari za ardhi 5000 huku kuna watanzania wanalalamika kwamba hawana ardhi na yupo mtanzania anayemiliki maekari mengi kama huyu ,huku bado akisema wazawa hawamiliki rasimali .Kweli toka hapo nikaamini hakuna tajiri kwenye nchi hii anayepigania maslahi ya taifa wala ya walalahoi kinachofanyika ni kujivika ngozi ya uzalendo kumbe ni walafi wanaongozwa na kusukumwa na maslahi yao binafsi.

Naomba watanzania tujiulize hawa sekta binafsi wakiongozwa na mwenyekiti wao ni kwanini walipigania wao wapewe upendeleo wa kupata vitalu kwanini wasingesema vitalu hivyo lipewe shirika la serekali la TPDC ambalo matunda yake yanarudi kwa umma wa watanzania. Hizo asilimia 10% wanazotaka wapewe na wawekezaji wa nje katika asilimia 35% wanazochukua wawekezaji ni kwanini kama ni kweli wazalendo ni kwanini hawakupiga kelele na kulia hizo asilimia ziongezwe kwenye asilimia za TPDC ili kuongeza asilimia kutoka 65 watazochukua ziwe 75. Kwani naamini faida ya TPDC kama itasimamiwa vizuri manufaa yatakuja kwa watanzania.Hata wakileta hoja kwamba serekali ya CCM haitoweza kusimamia mbaka manufaa kuja kwa watanzania wote je ? wanataka kutuaminisha kwamba wao hawaamini kwamba ipo siku nchi hii itashikwa na vyama  va  upinzani wanavyovisaidia kwa hali na mali ili vije kulinda maslahi yao baada ya kuona CCM haiwapi.Kwa kumalizia zaidi kama hawa matajiri wa ndani ni wazalendo na wanaoguswa na swala la ughali wa umeme katika nchi yetu inayochochewa na kusababishwa na umeme unaozalishwa na mafuta mazito ambayo ni ghali sana na yanaigharimu serekali mabilioni ya shilingi za kitanzania kuwanunulia makampuni yanayozalisha umeme kama vile IPTL kwa sasa PAP,SYMBION na AGRECO.Zaidi ya hayo makampuni yanayonunuliwa umeme pia serekali inanua mafuta hayo mazito kwa baadhi ya mikoa ambayo haijaunganishwa kwenye gridi ya taifa mikoa kama vile Kigoma na mingineyo.Ni wazi kwamba hawa matajiri wangekuwa wazalendo wa kutosha ni kwanini wasingeishauri serekali iongeze asilimia hizo kumi kufika 75 kitu ambacho kingeweza kutusaidia katika kupata gesi nyingi ambayo ingeweza kutusaida kuzalisha umeme mwingi wa gesi na kuepeuka gharama kubwa hii ya kununua mafuta mazito kwa mapesa mengi ya kitanzania ambayo yangeenda kusaidia katika shughuli nyiongine za Maendeleo kama afya,Elimu,miondominu ,kilimo na sekta nyingine yeyote nyeti kwa ajili ya Maendeleo ya watanzania walalahoi na watanzania wote. Kwa mazingira hayo inatuonyesha dhahiri kwamba hawa matajiri hawaguswi na uhaba wa umeme ambao kwa sasa tunazalisha MG 841 kitu ambacho ni chache sana kwasababu kwa nchi tu kama Norway yenye watu 4million wanazalisha MG 30000.Ni wazi kwamba kama matajiri wangekuwa wazalendo na wapigania maslahi ya umma na sio yao wangeishauri serekali iongee tena na wawekezaji waongeze asilimia kwenye zile 65 zitakazo chukuliwa na TPDC shirika la umma kwa manufaa ya uma.Kumbe nilichokiona ndugu zangu watanzania kwa hawa matajiri ni kwamba walitaka vitalu vya gesi wapate (wapige) pesa nyingi kwa kuuza hiyo gesi kwa serekali na kwengineko wanapopajua wao,familia zao na washirika wao wa ndani na nje ya nchi yetu inayotaka kuuliwa kwa maslahi ya wachache hawa .Kiufupi hawa walitaka kuwa mawakala ila sio wazalishaji na nashukuru Profesa Sospeter Muhongo aliwaambia ukweli bila ya kungata maneno .Na kwenye hili kusema kweli tunahitaji kiongozi shupavu kama yeye kwenye mazingira haya ambayo matajiri wa ndani na wa nje wanapambana kupigania maslahi yao kwa njia mpaka  za haramu zilizojaa chuki,dharau,kebehi na dhihaka .

Nimalizie kwa kusema kwamba watanzania ni lazima tuwe makini sana na hawa wanaojiita matajiri wazawa kumbe ni wasakatonge wazawa wenye kupigania maslahi yao ili hujifanya na kujinadi wanapigania maslahi ya taifa na watanzania  wote kwa ujumla. Hawa ni lazima tuwe nao makini sana kwani hawa ni hatari sana kwa mustakabali wa nchi yetu na ustawi wa maisha ya watanzania wote kwasababu hawa wanaendeshwa na falsafa ya “LIWALO NA LIWE ILA MASLAHI YETU NDIO KILA KITU” .Matajiri wa aina hii ni hatari sana wanaweza kuingiza nchi kwenye misukosuko hata ya machafuko ambayo yatasababisha maafa makubwa kwa walalahoi huku wao wakiwa wamepanda ndege kwenda nchi za nje kunywa wiski na bia. Ni muhimu pia kwa serekali kuchagua viongozi shupavu na wenye weledi wa hali ya juu wanaweza kupambana na hawa matajiri wasiokuwa na uzalendo hata kidogo na wanaotumia mali zao kupigania maslahi yao. Mfano wa viongozi wenye uwezo wa kupambana na hawa matajiri walafi, wabinafsi na wasioitakia mema taifa letu na wananchi wake wote tumeuona kwa Profesa Sospter Muhongo ambaye alikuwa Waziri wa Nishati na Madini Mchapakazi na Mwaminifu na Mwenye kila sifa na uwezo wa kuingoza wizara ile aliyokuwa anaiongoza na zaidi hata kuwa Rais wa nchi hii inayohitaji sayansi, teknolojia na uvumbuzi wa hali ya juu kwa ajili ya kuchochea kasi ya Maendeleo yetu yote.


Mwandishi wa Makala hii ni mimi Ismail Ramadhani .Muhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam shahada ya Sosholojia (Bachelor of Arts In Sociology and specialized in Social Policy and Administration) mwaka 2014.

Nashukuru Mungu nimemaliza vizuri Profesa Wangu na nimeliza na ufaulu wa G.P.A of 3.8 (Upper Second with Honours).

Ni miongoni mwa wachangiaji wa katika ule mjadala uliofanyika Nkurumah Hall “Uliokuwa unajadili juu ya umiliki wa rasilimali kwa watanzania” .Ni Yule kijana ninayeonekana nimevaa fulana ya nyeupe nikiwa nimeninginiza kitambulisho shingoni.



Nashukuru sana nimeandika makala hii leo hii baada ya kusoma makala yako ya “TANZANIA IJAYO: UFUGAJI WA KISASA NA BIASHARA KUBWA YA MAZAO YA MIFUGO YETU” inayoonyesha kwamba wewe ni msomi ambae kama taifa litakutumia vizuri hususani kwa ngazi kama ya Urais ukikosa kabisa uwaziri unaweza kulivusha taifa hili mbali sana .Mbali sana ambako Watanzania wengi wanatarajia kufika huko wakiamini kunaweza kunyanyua maisha yao yaliyoko kwenye lindi maskini .


“Asante sana Mungu Mbariki Profesa Sospeter Muhongo , Mpe nguvu ,afya ,hekima ,busara ,ujasiri ,uzalendo ,ujuzi utakaomfanya aweze kugombani urais wa nchi hii.Kama hatotaka Uraisi mpe moyo wa kugombania Ubunge hususani wa Musoma na mjalie ushindi.Huku Mungu ukinajalia mimi kuwa katika timu yake yakupigania na kushuhudia ushindi wake wa kishindo”.

Ameen

“Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika”

Asanteni Sana





Ismail Ramadhani

My Phone Number: o653 493732 

Email: ramadhanimatemanga@yahoo.com



No comments: