Advertisements

Wednesday, July 29, 2015

NGOMA AFRICA BAND YAFUNIKA INTERNATIONAL AFRICAN FESTIVAL TÜBINGEN 2015

Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa band maaruka kama FFU-Ughaibuni au viumbe wa ajabu Anunnaki Alien's inayoongozwa na kamanda Ras Makunja,bendi hiyo yenye makao yake kule ujuerumani ,juzi iliuhakikishia ulimwengu tena kuwa mziki wao ni moto wa kuotea mbali! bendi hiyo ilifanikiwa kwa mara nyingine kuyafunika maonyesho ya kimataifa ya International African Festival-Tübingen 2015,yaliofanyika katika viwanja vya Fest Platz,jijini Tübingen,Ujerumani.
Bendi hiyo ilipanda jukwaani majira ya saa 4.00 usiku huku uwanja huo ukiwa umezungukwa na ulinzi mkali ! kamanda Ras Makunja akikiongoza jukwaani kikosi chake kilichoshamili vijana wa kazi akina Afande Mo Benda (Soloist) Sajent JoJo Sousa(Drumer) Kopro. Aj Nbongo (Bass) kijana Liga (Rhthym guitar) madansa Jessica Ouyah na Sarah Fina kikosi hiko kilifanya show la kukata na shoka.siku ya jumamosi 26 Julai 2015.
wapitie at www.facebook.com/ngomaafricaband wasikilize at www.reverbnation.com/ngomaafricaband



No comments: