Chama cha wafanyakazi madereva Tanzania-TADWU-
kimetangaza mgomo wa madereva nchi nzima kuanzia Agosti tisa mwaka huu baada ya
wamiliki wa mabasi, wakala wa usafiri wa nchi kavu na majini pamoja na wizara
ya kazi kushindwa kutekeleza makubaliano yalifikiwa na tume iliyoundwa na
waziri mkuu kutatua mgogoro wa madereva nchni.
Kauli hiyo imetolewa na naibu katibu mkuu wa
TADWU, Bwana Rashidi Salehe wakati akizungumza na ITV ambapo amesema mgomo huo
unarejea tena baada ya wamiliki wa mabasi kwa kushirikiana na wizara kazi
pamoja na Sumatra kuendelea kutumia mikataba ya zamani katika kutoa leseni
wakati makubaliano ya tume iliyoundwa na waziri mkuu yalitaka mikataba mipya
ianze kutumika kuanzia julai mosi mwaka huu.
Wakizungumza na ITV baadhi ya madereva
wamelalamikia wizara ya kazi na sumatra kwa kukaidi agizo la waziri mkuu na
kuendelea kupokea mikataba ya zamani toka kwa wamiliki wa mabasi na kutoa
leseni wakati makubaliano yalishafanyika na kusisitiza katika makubaliano hayo
mishahara ya madereva wa malori yanayotoka nje ya nchi walikuwa wanatakiwa
kulipwa mishahara ya shilingi milioni moja, huku madereva wa daladala shilingi
laki tano pamoja na posho nyingine.
Akizungumza kwa simu na mmoja wa viongozi wa chama cha wamiliki wa mabasi nchni kwa masharti ya kutotajwa jina amewalalamikia madereva hao kwa kupanga mgomo badala ya kupeleka madai yao kwa tume ya kudumu iliyoundwa na waziri mkuu ili kupata ufumbuzi ambapo amesema kuna baadhi ya madereva wanatengeneza migomo ili kuleta usumbufu kwa wananchi na serikali kwa ujumla.
No comments:
Post a Comment