Advertisements

Saturday, August 29, 2015

DK. SHEIN AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA HOSPITALI YA ABDALLAH MZEE MKOANI PEMBA

Mchoro wa Majengo ya hospitali Mpya ya Abdallah Mzee Mkoani Pemba likiwa katika ujenzi wake kisiwani Pemba likiwa karibu asilimia 75 liko tayari na ujenzi wake.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Balozi Mdogo wa China Zanzibar Balozi Xie Yunliang, alipowasili katika viwanja vya hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali, Mohamed Shein, akisalimiana na Kiongozi wa Madaktari wa Kichina Dr. Xu Zhuogun alipowasili katika viwanja vya ujenzi wa Hospitali Mpya ya Abdalla Mzee Mkoani jana kwa kuweka jiwe la Msingi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar alipowasili katika viwanja vya ujenzi wa hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani jana.
Rais wa Zanzibar akisalimiana na Madaktari wa Kichina katika viwanja vya ujenzi wa jengo jipya la hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani jana.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mkalimali wa Kampuni ya Ujenzi ya Kichina Zhang Dov.inayojenga hospitali hiyo
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akiondoa kipazia kuashiria kuweka jiwe la msingi la jengo jipya la Hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani jana.













Kwa hisani ya ZanziNews

1 comment:

Anonymous said...

Wachina oyeee!! Kweli Tanzania itaendelea kwa mwendo huu!!!