ANGALIA LIVE NEWS

Thursday, September 24, 2015

KUFUATIA KURIPOTIWA UGONJWA WA KIPINDUPINDU KUINGIA MANISPAA YA DODOMA WANANCHI BADO HAWAJAWA NA ELIMU JINSI YA KUKABILIANA NAO

  Baadhi ya  akina mama na watoto wao wakitafutia chochote katika Dampo ambalo si Rasmi lililopo pembezoni mwa Barabara ya 12 karibu na kituo cha Daladala ziendazo Nkuhungu Jamatini bila kujali maambukizi ya magonjwa, huku wahusika wakioneka kutokujali



wakati ugonjwa wa kipindupindu ukiwa unazidi kushika kasi  katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam huko mkoani dodoma nako inasadikika kwamba ugonjwa huo umekwisha gonga hodi huku wakazi wa maeneo mbalimbali wakionekana kusambasa hovyo uchafu na wengine kuwa katika sehemu hatarishi za kuweza kupata ugonjwa huo
katika barabara ya kumi na mbili (12) huko mkoani Dododma pembezoni kidogo mwa barabara kumeonekana baadhi ya wakazi wa mji  huo wakiwa katika sehemu za kutupia taka  na kuzihifadhi kwaajiri ya kuzichoma arimaarufu kama (Dampo) bila kuogopa tahadhari ya ugonjwa wa kipindupindu ,licha ya serikali kila siku kupiga kelele kuhusiana na usafi na utunzaji wa mazingira   wa miji yetu hali imekuwa tofauti na mapokeo ya wananchi kwani wamekuwa wakikaidi na kuweka taka hizo sehemu zisizo stahili bila kujali afya zao 
Tunza mazingira ili uepukane na magojwa ya mlipuko epuka uchafu ili uwe na afya bora

No comments: