Mwenyekiti wa makampuni ya Quality group, Yusuf Manji ameibuka mshindi wa tuzo maarufu ya Mfanyabiashara Gwiji Duniani.
Manji ambaye ni mwenyekiti wa mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga ameibuka mshindi wa tuzo hiyo na kuwashinda mabosi wengine kama bilionea namba moja Afrika Aliko Dangote.
Kwa mujibu wa mtandao wa Business Forum, Mwenyekiti huyo wa amekuwa kiongozi wa kwanza kutoka Afrika kushinda tuzo hiyo ambayo awali walikuwa wakichukua matajiri wengine wakubwa na maarufu kutoka katika mabara ya Amerika, Ulaya na Asia.
Msemaji wa Quality Group, Smitha Swamy jana alithibitisha Manji kushinda tuzo hiyo, lakini akasema atakuwa tayari kulizungumzia hilo, leo.
“Ni kweli, lakini leo nimebanwa. Nitalizungumzia hilo kesho,” alisema.
Baadhi ya waliowahi kutwaa tuzo hiyo ni Mwenyekiti wa Emirates Group, Sheikh Ahmed bin Saeed Al Maktoum inayomiliki kampuni ya Ndege ya Emirates inayozidhamini timu za Real Madrid, Arsenal, AC Milan na nyingine kubwa.
Wengine ni Mwenyekiti wa Emmar Properties, Mohammed Alabbar pia bilionea kutoka India, Ratan Tata anayemiliki kampuni kubwa ya Emeritus of Tata Sons Ltd.
Pia bilionea aliye tano bora duniani kwa utajiri, Mukesh Ambani ambaye ni mwenyekiti wa Reliance Industries Ltd. Wengine ni Yingluck Shinawatra, Waziri Mkuu wa zamani wa Thailand.
Pamoja na ushindi huo wa kishindo wa Manji dhidi ya matajiri wengine wakubwa Afrika na duniani kote, Kampuni yake ya Quality Group imeshinda kuwa kampuni bora na yenye mpangilio wa uhakika kwa bara la Afrika ikipewa tuzo ya “Most Iconic Brand 2015”.
Source :SALAHJEMBE
1 comment:
HIYO TUZO INATOLEWA NA NANI,WAPI,INA NINI NDANI YAKE,HUPOKELEWA VIPI,NANI HUWA MGENI WA HESHIMA,JEE HII SIYO KAMPUNI TANZU YA QUALITY GROUP ILIYOPO ONTARIO,CANADA,INA MAANA GANI KWA NCHI YETU NA MTANZANIA WA KAWAIDA?NISAIDIWE NA WAELEWA WA KWELI WANIELIMISHE VINGINEVYO NAONA KAMA PR VILE, KWA MALENGO YA KISIASA NA KUJINYANYUA BILA KUNYANYULIWA.
Post a Comment