Saturday, October 24, 2015

BALOZI WA TANZANIA NCHINI MALAWI, AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO

Tarehe 22 Oktoba, 2015 Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege alipata fursa ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Prof. Arthur Peter Mutharika katika Ikulu ya Kamuzu Palace mjini Lilongwe.
Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege akipigiwa nyimbo za taifa za Malawi na Tanzania huku akishuhudiwa na maafisa Ubalozi.
Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege akikagua gwaride lililoandaliwa kwa heshima yake
Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Kamuzu Palace mjini Lilongwe. Wanaoshuhudia ni maafisa Ubalozi Wilbroad A. Kayombo kushoto, Elyneema Lissu, Nimpha Marunda na Mbonile Mwakatundu
Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais Prof. Arthur Peter Mutharika
Maafisa Ubalozi wakitambulishwa kwa Mhe. Rais Prof. Arthur Peter Mutharika
Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege na Mhe. Rais Prof. Arthur Peter Mutharika wakitoka nje baada ya mazungumzo
Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege akiagana na Mhe. Prof. Arthur Peter Mutharika 
Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege akiondoka Ikulu mara baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho
 
Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege akiagana na Afisa wa Itifaki Bw. Miller Chizukuzuku mara baada ya kuwasili nyumbani
Watumishi wa Ubalozi wakiwa na Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege nyumbani kwake

No comments: