Advertisements

Wednesday, October 7, 2015

MAGUFULI AZIDI KUIBOMOA CHADEMA KILIMANJARO,AWATOLEA UVIVU WATENDAJI WA SHIRIKA LA UMEME NCHINI

 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Moshi mjini Ndugu Davis Mosha kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Mashujaa,mkoani Kilimanjaro jioni ya leo.PICHA ZOTE NA MICHUZI JR-KILIMANJARO.
  Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli akisisitiza jambo alipokuwa akihutubia umati wa Wananchi wa mji wa moshi waliofika katika viwanja vya mashujaa Kumsikiliza alipokuwa akijinadi na kuwaga sera zake katika kuomba kura za kuwania nafasi ya Urais kwa kipindi cha awamu ya tano,kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.
 Sehemu ya Umati wa Wananchi wa mji wa moshi waliofika katika viwanja vya mashujaa wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,leo jioni kwenye mkutano wa kampeni,mkoani Kilimanjaro alipokuwa akijinadi na kuomba kura za kutosha ili aibuke kuwa Rais wa Tanzania wa awamu ya tano,katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.
 Mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli na mgombea ubunge wa jimbo la Moshi mjini Ndugu Davis Mosha wakimsikiliza Bw. Lema aliyekuwa Katibu wa Chadema wilaya ya Hai wakati alipojiunga na CCM katika mkutano huo.

 Mgombea Urais wa CCM Dkt Jonh Pombe Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa CCM ndani ya jimbo la Arumeru Mashariki,ndugu John Daniel Pallangyo,kweye mkutano wa kwampeni uliofanyika katika uwanja wa Ngareselo (USA River),jijini Arusha.

 Mmoja wa wajumbe wa timu ya ushindi ya kampeni za CCM,Dkt Emmanuel Nchimbi akimnadi Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,kweye mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa CCM,Sanya Juu,mkoani Kilimanjaro.
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Siha,Ndugu Aggrey Mwanri mbele ya wakazi wa Siha (hawapo pichani),waliokuwa wamekusanyika katika uwanja wa CCM kwenye mkutano wa kampeni

Sehemu ya Umati wa Wananchi wa mji wa moshi waliofika katika viwanja vya mashujaa wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,leo jioni kwenye mkutano wa kampeni,mkoani Kilimanjaro.
Magufulika Style  inavyozidi kushika kasi,Davis Mosha mgombea ubunge jimbo la Moshi mjini na madiwani wa Moshi mjini wakimagufulika jukwaani kuonyesha ukakamavu wao.
 Sehemu ya Umati wa Wananchi wa mji wa moshi waliofika katika viwanja vya mashujaa wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,leo jioni kwenye mkutano wa kampeni,mkoani Kilimanjaro.

Katika mkutano wake wa Moshi mjini Dkt. Magufuli amewaonya watendaji wa Shirika la Umeme nchini TANESCO na kuwaambia kama wanazima umeme makusudi ili kuwafanya wananchi waichukie serikali wanafanya makosa na ole wao kwa vitendo hivyo visivyo vya kistaarabu, Amewaambia kwamba bado siku 17 za kampeni akichaguliwa na wananchi na kuapishwa kuwa Rais atawashughulikia ipasavyo kwani  wanajulikana.  “Katika siku hizi zilizobaki watubu wafanye kazi usiku na mchana ili umeme upatikane bila kukatika na kuleta adha kwa wananchi vinginevyo akiingia Ikulu atalala nao mbele”,alisema Dkt Magufuli huku uwaja mzima ukilipukwa kwa mayowe.
 Sehemu ya Umati wa Wananchi wa mji wa moshi waliofika katika viwanja vya mashujaa wakimsikiliza Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,leo jioni kwenye mkutano wa kampeni,mkoani Kilimanjaro.
 Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli akihutubia umati wa Wananchi wa mji wa moshi waliofika katika viwanja vya mashujaa Kumsikiliza alipokuwa akijinadi na kuwaga sera zake katika kuomba kura za kuwania nafasi ya Urais kwa kipindi cha awamu ya tano,kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.
 Mgombe Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akisoma mabango aliyokuwa yamebebwa na baadhi ya wafuasi wa chama cha CCM,wakati akiwasili kwenye uwanja wa mkutano wa kampeni ndani ya jimbo la Arumeru Mashariki (Usa river),uliofanyika katika uwanja wa Ngareselo mkoani Arusha.
Baadhi ya wakazi wa USA River wakiwa wamekusanyika kwenye uwanja wa mkutano wa kampeni ndani ya jimbo la Arumeru Mashariki,katika uwanja wa Ngareselo,kumsikiliza  Mgombe Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akijinadi sera zake 
 Kiongozi wa Msafara wa Kampeni za Mgombea Urais wa CCM,Ndugu Abdallah Bulembo akisalimiana na kada wa CCM,aliyekuwa mkuu wa kwanza wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jenerali Mirisho Sarakikya huku Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufulia akishuhudia tukio hilo
 Baadhi ya wakazi wa USA River wakiwa wamekusanyika kwenye uwanja wa mkutano wa kampeni ndani ya jimbo la Arumeru Mashariki,katika uwanja wa Ngareselo,kumsikiliza  Mgombe Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akijinadi sera zake za kuomba kuwania nafasi ya Urais.
  Baadhi ya wakazi wa USA River wakishangilia jambo kwenye uwanja wa mkutano wa kampeni ndani ya jimbo la Arumeru Mashariki,katika uwanja wa Ngareselo,wakati Mgombe Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akijinadi sera zake na kuomba kuwania nafasi ya Urais.
 Wananchi wa wilaya ya Siha wakimsikiliza Mmoja wa wajumbe wa timu ya ushindi ya kampeni za CCM,Dkt Emmanuel Nchimbi alipokuwa akimnadi Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,kweye mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa CCM,Sanya Juu,mkoani Kilimanjaro.
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli,akijinadi mbele ya wakazi wa wilaya ya Hai,kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye stendi ya Malori ndani ya mji wa Boma ng'ombe,mkoani Kilimanjaro
 Mgombea Urais wa CCM Dkt Jonh Pombe Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo Moshi Vijijini Dkt Cyril Chami pamoja na madiwani ndani ya mji wa Uru Shimbwe,kwenye mkutano wa kampeni

10 comments:

Anonymous said...

Ahadi ya viwanda vifufuliwe ndani ya siku 17 hizi ni ndoto hata kichaa hawezi kukubali. Hivi umeviona vilivyo magofu. Na hao waajiriwa ni wepi hao ambao wameenda shule au watoke huko barabarani walala hoi!! Vinatakiwa kuandaliwa sio ahadi kukurupuka!! Hatikubaliani na hilo..

Anonymous said...

Huyu mwandishi wa nakala ni wazi ni mpenzi mkubwa wa CCM, ukiangalia jinsi amekuwa akiandika vichwa vya habari vya Magufuli na Lowassa ni tofauti kabisa.

Anonymous said...

Sema hukubaliani na hilo sio hatukubaliani na hilo mi nakubaliana na hilo haya nawewe toa sera za Lowasa kuuchukia umaskini atawapa utajiri kila mtu ndio sera,,,, piga kimya masela wangu CCM chama kubwa.

Unknown said...

Mdau wa anonymous wa oct 7,2015 at 8:11pm.

Wewe ndie mwenye kichaa tena wa kutembea bila ya nguo, muheshimiwa magufuli amezungumzia suala la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika wakati huu wa kampeni. Na kuendelea kuelezea kwamba hao watumishi wa shirika la umeme warekibishe hilo suala linalo sababisha umeme kukatika mara kwa mara kabla siku 17 za uchaguzi kwani akiingia madarakani hao wababaishaji wa shirika la umeme wajiandae kutafuta kazi nyengine.
Sasa kiwanda gani unachozungumzia ? Wewe mtu mwenye elimu wa kiwango cha PhD na uzoefu wa zaidi miaka 20 ya kazi uliotukuka unataka kumlishia maneno ya kipumbavu. Yaani sera kubwa ya ukawa ni upotoshaji na propaganda zisiozokuwa na mishiko ya aina yeyote lakini kwa magufuli mnanyooka tu.

Anonymous said...

Haya wacha tuendelee kudanganywa, yaani watanzania kweli sio bure

Anonymous said...

Haya wacha tuendelee kudanganywa, yaani watanzania kweli sio bure

Anonymous said...

Mungu wasaidiee watanzania ambao hawajui lile watendalo, shida na tabu zote wanazozipata wamezisahau kwa dakika moja, haya tutafika tu

Anonymous said...

Hukuambiwa viwanda vitaanza kufanyakazi ndani ya siku 17.

Anonymous said...

You're probably functionally illiterate! If you cannot comprehend such short passages, you surely shouldn't be expressing any opinion.

Anonymous said...

Waswahili walisema, "akili nyingi huondoa maarifa" ndiyo maana watu wenye akili nyingi bila maarifa wanashindwa kuelewa wanayoyasoma.

Hapa kazi moja tu.Magufuli Ikulu 10/25/2015.