Advertisements

Wednesday, October 28, 2015

Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Ufilipino

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Ufilipino nchini Tanzania mwenye makazi nchini Kenya, Mhe. Bayani V. Mangibin. Hafla hiyo imefanyika Ikulu Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2015. 
Balozi Mangibin akizaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam 
Balozi Mangibin (kulia) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberatta Mulamula (kushoto) mara baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais Jakaya Kikwete (katikati mwenye tai nyekundu) 
Balozi Mangibin (kulia) akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Khatibu Makenga (wa kwanza kushoto) alipokuwa akitambulishwa na Mhe. Rais. 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga (wa kwanza kushoto) akisalimiana na Balozi Mangibin (kulia). 
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mangibin. 
Picha ya pamoja 

Picha na Reginald Philip

No comments: