Advertisements

Wednesday, October 28, 2015

Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Israel

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Balozi mpya wa Israel hapa nchini mwenye Makazi yake nchini Kenya, Mhe. Yahel Vilan mara baada ya kupokea Hati zake za utambulisho. Hafla hiyo imefanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2015. 
Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Balozi Vilan, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula. 
Balozi Vilan akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Elibariki Maleko. 
Balozi Vilan akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga 
Balozi Vilan akisalimiana na Bw. Batholomeo Jungu, Afisa Mambo ya Nje 
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Vilan 
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Vilan na Balozi Mulamula 
Balozi Elshawaf (katikati) akipokea heshima ya wimbo wa taifa mara baada ya kuwasili Ikulu. Kulia ni Mkuu wa Itifaki Balozi Juma Maharage na kushoto Mnikulu. 
Bendi ya polisi ikipiga wimbo wa taifa wa Misri kwa heshima ya Balozi Elshawaf 
Balozi Elshawaf akisalimiana na Bw. Celestine Kakele, Afisa Mambo ya Nje 
Balozi Elshawaf akisalimiana na Kiongozi wa Bendi ya Polisi 


Picha na Reginald Philip

No comments: