ANGALIA LIVE NEWS

Thursday, November 5, 2015

Viongozi mbalimbali waendelea kuwasili kwaajili ya sherehe za Uapisho wa Rais Mteule

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (kushoto) akimpokea Rais wa Afrika ya Kusini Mhe. Jacob Zuma (anayeshuka kwenye ngazi), Rais Zuma amewasili nchini kwaajili ya kuudhuria sherehe za uapisho wa Rais Mteule Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli zitakazofanyika hapo kesho katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam 
Waziri Membe akisalimiana na Rais Zuma 
Rais Zuma akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Mhe. Radhia Msuya (wa kwanza kulia). 
Rais Zuma akitizama kikundi cha ngoma kilichokuwa kikitoa burudani. 
Balozi wa Tanzania nchini UAE Mhe. Mbarouk Nassoro Mbarouk (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Maendeleo ya Jamii UAE. 
Afisa Mambo ya Nje Bw. Hangi Mgaka naye akisalimiana na Waziri wa Maendeleo ya Jamii UAE 

Picha na Reginald Philip.

No comments: