Mabondia Shedrack Ignas kushoto akitunishiana misuli na Abdallah Luwanje baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga januari 2 katika ukumbi wa frends corner manzese
Na Mwandishi Wetu
MABONDIA mbalimbali wa ngumi za kulipwa wamesaini mkataba wa mpambano wa kufungua mwaka kuzipika siku ya januar 2 mwakani katika ukumbi wa frends corner manzese Dar es salaa
akizungu wakati wa kusaini mikataba hiyo mratibu wa mpambano uho Rajabu Mhamila 'Super D' amesema kuwa mabondia walio wasainisha kuwa ni Shedrack Ignas atakaepambana na Abdallah Luwanje na
Hassan Salumu atakabiliana na
Hassan Mgosi nae Shomari Mirundi atapambana na Husein Mbonde na Ramadhani Maonya atakumbana na Said Faraji wakati Kelvin Majiba atakumbana na Ibrahimu Hamis mabondia wengine walio saini ni Mohamed Muhunzi na Mohamed Kashinde
mpambano huo ulioandaliwa na kampuni ya Butamanya General Tredes and Boxing Promotion
imeandaa mpambano huo kwa ajili ya kukuza viwango vya mabondia chipkizi na kuimalisha zaidi wale wenye uwezo kwa ajili ya kuwapatia mipambano mbalimbali ya ndani na nje ya nchi
Super D aliongeza kwa kusema kuwa siku hiyo kutakuwa na burudani za nguvu pamoja na ulinzi wa kutosha na ngumi zitaanza mapema ili wapenzi wa mchezo wa masumbwi warudi majumbani mapema wakiwa na furaha ya mchezo utakaochezwa
No comments:
Post a Comment