Sunday, December 6, 2015

Tanesco yawafukuza kazi wafanyakazi 7 kwa ubadhilifu

Uongozi wa shirika la umeme nchini Tanesco umewafukuza kazi wafanyakazi saba waandamizi wa shirika hilo wakiwemo mameneja kutokana na makosa mbalimbali ikiwemo vitendo vya wizi, kudai rushwa, ubadhirifu wa mali wa shirika hilo pamoja na kutoa lugha chafu kwa wananchi jambo ambalo ni kinyume na taratibu za maadili ya kazi na uongozi huo kuwaonya wafanyakazi wengine wenye tabia kama hizo kwamba watachukuliwa hatua.

Mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Mhandisi Felichesm Mramba akitoa taarifa juu ya uumuzi wa kufukuzwa kazi kwa wafanyakazi hao saba kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam amesema uamuzi huo umechukuliwa ikiwa ni mpango endelevu wa shirika la Tanesco kuimrisha nidhamu kwa wafanyakazi wake kutambua wajibu wao wa kutoa huduma ya nishati kwa wananchi na sio na sio kuwasumbua wateja na kutaja vitengo ambavyo wafanyakazi hao wamefukuzwa ikiwemo ngazi ya mameneja, wahandisi na wahasibu kutoka mikoa ya Kinondini kaskazini, Katavi, Kagera na Ilala.

Akiendelea kutoa taarifa juu ya utekezaji wa kusanyaji wa mapato ili kuendesha shirika hilo kwa ufanisi unaotakiwa kwa sasa mhandisi Mramba ametoa siku saba kwa wateja ambao wanalihujumu shirika la umeme kwa kujiunganishia umeme kwa wizi kujisalimisha wao wenyewe kutokana na kuanza kwa operesheni maalumu ya nyumba kwa nyumba kuhakiki mita ili kubaini upotevi wa nishati ya umeme inayotumika bila kulipiwa mpango ambau utahusisha jeshi la polisi katika kuwakamata wahalifu wote na mali zao sasa kunadiwa wakishindwa kulipa faini.

Pamoja na mambo mengine mkurugenzi mkuu huyo wa Tanesco amesema mpango wa uzalishaji wa nishati ya umeme kwa kutumia vyanzo vya gesi tokea mwezi septemba mwaka huu umesaidia kuongeza megawati 300 kutoka megawati 260 hivyo hatua hiyo kuchangia kuboresha hali ya umeme hapa nchini na kuwa na matarajio ya kupata megawati 700 ifikapo mwezi januari mwakani kupitia umeme wa nishati ya gesi.

CHANZO:ITV

2 comments:

Anonymous said...

sawa,lakini zingatieni taratibu na sheria.yaani msiwe waoga kupindukia kwa minajiri ya kujikosha kwa mheshimiwa magufuli.kama hamzingatii taratibu na sheria,watumishi hawa watafungua mashauri mahakamani na mwisho wa siku mkajikuta mnawalipa fedha nyingi mno,na kisha nyinyi sasa mje mfukuzwe kwa uzembe wa kulitia shirika hasara!

Anonymous said...

Mtafukuza wengi
Lakini siyo solution
Lazima tubadili mfumo mzima kuanzia tume ya uchaguzi
Usalama WA raifa
Jeshini la wanainchi tanzania
Polisi
Huwezi tu kufukuza watu waskini walikuwa wakitimiza matakwa ya waliowaweka madarakani
Magufuli nenda nyuma wewe unaweza kumuweka ndani mwinyi, mkapa, na kiwetwe
Ukiwaona wana hatia