Wednesday, January 6, 2016

WAZIRI MKUU ASEMA SERIKALI HAIJARIDHIA VIWANGO VIPYA VYA NAULI YA MABASI YAENDAYO KASI.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizunguza na Waandishi wa Habari kwenye uwanja wa Ngege wa Julius Nyerere baada ya kuwasili akitoka Songea Januari 6, 2016. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Geoge Simbachawene. na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es slaam Meck Sadiki.


Baadhi ya waandishi wa habari wananchi wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere baada ya kuwasili akitoka Songea Januari 6, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali haijaridhia viwango vipya vya nauli ya mabasi yaendayo kasi vilivyopendekezwa na waendeshaji wa huduma ya mabasi yaendayo kasi Dar es salaam (UDART).
Akizungumza leo na waandishi wa habari, mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam akitokea mkoani Ruvuma kwa ziara ya siku 3, Waziri Mkuu amesema Serikali haijaridhia viwango vipya vya nauli ya mabasi yaendayo kasi. Ambapo nauli ya kutoka Mbezi hadi Kimara shilingi 700, Mbezi hadi Kariakoo shilingi 1200, na nauli ya kutoka Mbezi hadi Mwenge shilingi 1400 na wanafunzi watatozwa nusu ya viwango hivyo vya nauli. 
Waziri Mkuu amesema gharama hizi ni kubwa mno kwa wananchi na watumishi, mradi ulilenga kumrahisishia mtumishi wa Serikali anayeishi nje ya jiji, “Serikali iliwekeza katika mradi huu ili kusaidia watumishi na wananchi ambao hawana vipato vikubwa” alisema Waziri Mkuu. 
Aidha, ameagiza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa George Simbachawene na Waziri wa Ujenzi , Uchukuzi, na Mawasiliano pamoja na wadau wakutane kupanga upya viwango hivyo na kama watashindwa basi Serikali itaendesha mradi huo. 
Tarehe 25, Novemba 2015, Waziri Mkuu alimuagiza aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya TAMISEMI na waendeshaji wa mradi wa mabasi yaendayo kasi Dar es salaam (UDART) kupitia misuada yote na kurekebisha miundombinu ili mradi huo wa mabasi uanze kufanya kazi ifikapo tarehe 10, Januari 2016, imebainika kwamba UDART hawakuandaa mpango wa biashara wala kuanisha gharama za uendeshaji.

3 comments:

Anonymous said...

mheshimiwa majaliwa,salaam.kwa mara kadhaa katika utendaji wa kazi zako umekuwa ukitoa amri za kiutendaji.sasa hili la hawa DART kujipangia nauli kubwa na ya kutisha mbona umeshindwa kulitolea amri ya kufuatwa.mimi nilitegemea utasema,'kuanzia leo nauli mpya zilizopendekezwa na DART ni haramu serikali inaagiza nauli kuwa 400 kama ilivyo nauli ya dala-dala.wakishindwa,wasitoe huduma,wapeleke mabasi yao mikoani kwenye nauli za masafa'.hii ingependeza zaidi.madhara ya kupandisha nauli ni makubwa mno kisiasa,kiuchumi na kisaikolojia.

Anonymous said...

Ninapata wasix2 na uhai wa mradi huu siasa inapoingia ndani ya biashara Uhai wake ni mdogo.Historia ni shahidi,serikali yetu haina rekodi nzuri ya kuendelea biashara. i.e UDA,Air Tanzania, Migodi etc

Anonymous said...

Serikali isitake kuuendesha huu mradi kama NGO utakufa muda si mrefu.