Tuesday, January 5, 2016

WIZARA YA MAJI YAMUAGA NAIBU KATIBU MKUU INJ. MWIHAVA, YAMKARIBISHA INJ. KALOBELO

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Inj. Emmanuel Kalobelo akipokea nyaraka  kama ishara ya kukabidhiwa rasmi ofisi kutoka kwa aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Inj. Ngossy Mwihava, wakishuhudiwa na Katibu Mkuu, Inj. Mbogo Futakamba.
Wizara ya Maji imemuaga rasmi aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Inj. Ngossy Mwihava na kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu mpya, Inj. Emmanuel Kalobelo katika Makao Makuu ya Wizara hiyo Ubungo Maji jana.
 “Naomba ushirikiano wenu ili tuweze kufanikisha azma ya kuleta maendeleo kwenye Sekta ya Maji, na nasisitiza kufanya kazi kwa bidii na kujituma kwetu sote ili tulete faraja kwa wananchi”, alisema Naibu Katibu Mkuu, Inj. Emmanuel Kalobelo katika hafla fupi ya kutambulishwa na makabidhiano ya ofisi.
 Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Inj. Ngossy Mwihava akizungumza na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Inj. Emmanuel Kalobelo ofisini kwake, kabla ya kumkabidhi ofisi.
 Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Inj. Mbogo Futakamba (katikati), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Inj. Emmanuel Kalobelo (kushoto), aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Inj. Ngossy Mwihava (kulia) na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Gideon Manambo.
 Naibu Katibu Mkuu, Inj. Emmanuel Kalobelo akizungumza na Menejimenti ya Wizara ya Maji mara baada ya kutambulishwa.
 Menejimenti ya Wizara ya Maji ikimsikiliza Katibu Mkuu, Inj.  Mbogo Futakamba alipokuwa akizungumza.

No comments: