Advertisements

Saturday, February 6, 2016

MAADHIMISHO YA CCM YAFANA SINGIDA, JK AMMGIA SIFA LUKUKI RAIS MAGUFULI, YEYE AAGIZA VIONGOZI WASIOTEKELEZA ILANI YA CCM AONDOKE

 Rais John Magufuli akiwasalimia wananchi baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa CCM Namfua, katika maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa CCM ambayo kitaifa yamefanyika leo mkoani Singida. Kutoka kulia ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye na Katibu Mkuu wa chama hicho, Abdulrahman Kinana.
 Rais Magufuli akiwapungia mkono wananchi.

 Rais Magufuli akisalimiana na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akijadiliana jambo na Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu pamoja na Nape Nnauye.
 Mwenyekiti wa CCM, Rais mstaafu Jakaya Kikwete akilakiwa na Katibu Mkuu wa CCM, Kinana alipowasili kwenye Uwanja wa CCM Namfua, mjini singida kuongoza maadhimisho ya miaka 39 ya CCM.
 Rais John Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM, UJakaya Kikwete
 JK akisalimiana na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan. Katikati ni Rais Magufuli.
 Mtoto Yusufu anayeandaliwa na babake kuwania urais 2050 akiwa kwenye baiskeli aliyotengenezewa na babake pichani.
 Mwanamuziki wa Bendi ya Yamoto Band akiwaimbisha wananchi wakati wa sherehe hizo.
 Bendi ya Yamoto ikitumbuiza wakati wa maadhimisho ya miaka 39 ya ccm kwenye Uwanja wa Namfua, Singida.
 Kikundi cha TOT kikitumbiza kwa wimbo maalumu wa maadhimisho ya miaka 39 ya CCM
 Watoto wakipiga mafataki kunogesha maashimisho hayo
 Rais Magufuli akimpongeza aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu Mashishanga kujiunga na CCM akitokea Chadema.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpongeza Cresto Haja aliihama Chadema na kujiunga na CCM
 Rais John Magufuli akimpongeza Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kwa hotuba yake wakati wa maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM, wakati wa maadhimisho yhayo yaliyofanyika kwenye Uwanja wa CCM Namfua, mjini Singida leo. Kutoka kushoto ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete na Samia Suluhu Hassan Makamu wa Rais.
Sehemu ya umati wa wananchi wakiwa katika maadhimisho hayo.

No comments: