Monday, February 29, 2016

WABUNGE HALIMA MDEE NA SAIDI KUBENEA WATAITIWA NA POLISI

Mbunge wa Kawe Halima Mdee.
Mbunge wa Ubungo, Said Kubenea.

Habari ambazo vijimambo imezipata Wabunge wa CHADEMA Mhe. Halima Mdee na Mhe. Saidi Kubenea wameshikiliwa na polisi jijini Dar kutokana na vurugu zilizotokea siku ya uchaguzi wa Meya uchaguzi ulikua ufanyike kwenye ukumbi wa Karimjee

Habari zingine zilizoandikwa na Mbunge wa CDM Arusha katika ukurasa wake wa facebook Mhe. Godbless Lema zime sema hakukua na zuio la mahaka ya Kisutu kuhusu uchaguzi wa meya hizo ni habari zilizotungwa na CCM katika kuzuia uchaguzi usifanyike, amri ya mwisho kutolewa na mahakama ilikua tarehe 23 Februari mwaka huu.

Baada ya tamko hilo la mahakama Jeshi la Polisi limeanza kuakamata wabunge wa CHADEMA akiwemo diwani wa Kimara Bwn. Ephrahim Kinyafu

Bofya hapo chini usome ujumbe ulioandikwa na Mhe. Godbless Lema kwenye ukurasa wake wa facebook



No comments: