Advertisements

Thursday, June 23, 2016

Katibu Mkuu wa AALCO, Prof. Gastorn afanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga )(Mb) kulia akifanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Mashauriano ya Masuala ya Kisheria katika Nchi za Asia na Afrika (Asian – African Legal Consultative Organization (AALCO), Prof. Kennedy Gastorn. Prof. Gastorn alichaguliwa kushika nafasi hiyo wakati wa Mkutano wa 55 uliofanyika mjini New Delhi, India mwezi Mei 2016. Prof. Gastorn alikuja kumuona Mhe. Waziri kwa lengo la kujitambulisha, kushukuru kwa kuungwa mkono na kubadilishana taarifa kuhusu Jumuiya hiyo.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Mashauriano ya Masuala ya Kisheria katika Nchi za Asia na Afrika (Asian – African Legal Consultative Organization (AALCO), Prof. Kennedy Gastorn akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo hayo. Alibainisha kwamba nafasi hiyo ni heshima kubwa kwake na nchi kwa ujumla kwa kuwa jukwaa hilo ni jukwaa muhimu kwa maendeleo ya sheria za Kimataifa nchini na Barani Afrika. Aliiomba Serikali ya Tanzania kuendelea kumuunga mkono kwenye utekelezaji wa majukumu yake kwa kuzisihi nchi za Afrika zijiunge na AALCO. 
Mhe. Waziri akiendelea na mazungumzo yake ambapo alitoa pongezi kwa Prof. Gastorn na kumtakia kila la kheri kwenye utekelezaji wa majukumu yake mapya na kumuahidi ushirikiano wa Serikali ya Tanzania. Wengine katika picha ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Baraka Luvanda (tai nyekundu) na Afisa wa Kitengo hicho, Bw. Abdallah Mtibora.

No comments: