Advertisements

Thursday, June 23, 2016

MRADI WA PS3 WAENDESHA MAFUNZO KWA MAAFISA WASIMAMIZI RASILIMALI WATU KATIKA KUPATA MBINU ZA KUFUNDISHI WATUMISHI

Mkurugenzi wa Mradi wa PS3 Dk. Emmanuel Malangalila akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili yaliyo wakutanisha pamoja wataalam mbalimbali wanaohusika na usimamizi wa rasilimali watu kutoka katika mikoa na tasisi za serikali ili kupata kitini cha kutolea mafunzo kwa watumishi wapya wanaoajiriwa serikalini. Mafunzo hayo yanafanyika mjini Bagamoyo mkoani Pwani. 

Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3) nchini ambao unatekelezwa katika mikoa 13 na kuzinufaisha halmashauri 97. 
Baadhi ya maofisa kutoka Ofisi ya Rais, tawala za Mikoa na serikali za Mitaa (TAMISEMI). Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Serikali za Mitaa, Miriam Mmbaga akifuatiwa na Beatice  Kimoleta

Washiriki wa mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo wasimamizi wa rasilimali watu katika taasisi na Halamashauri mbalimbali nchini. Mafunzo hayo yanalenga kuwaweza waajiri hao kutafuta mbinu ikiwepo mafunzo na motisha mbalimbali kwaajili ya kuwafanya watumishi wapya wanapoajiriwa kuendelea kufanya kazi katika mazingira yeyote. 
Mkuu wa Kitengo cha Mifumo ya Rasilimali wa Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3)  Josephine Kimaro akitoa mafunzo kwa viongozi wa sekta ya Afya waliojitokeza kushiriki semina hiyo mjini Bagamoyo mkoani Pwani. 
Washiriki wa mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo wasimamizi wa rasilimali watu katika taasisi na Halamashauri mbalimbali nchini. Mafunzo hayo yanalenga kuwaweza waajiri hao kutafuta mbinu ikiwepo mafunzo na motisha mbalimbali kwaajili ya kuwafanya watumishi wapya wanapoajiriwa kuendelea kufanya kazi katika mazingira yeyote. 
Mkurugenzi wa Mradi wa PS3 Dk. Emmanuel Malangalila (kushoto) akiwa na washiriki wengine wakifuatilia mada katika mafunzo hayo. 
Mshauri wa masuala ya Rasilimali watu kutoka PS3, Sheillah Matinhure akiwasilisha mada juu ya mafunzo ya awali na kuwaingiza kazini watumishi wappya pamoja na kupokea changamoto kutoka kwa viongozi wa Serikali za Mitaa. 
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Serikali za Mitaa kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Miriam Mmbaga akiwasilisha mada. 
Washiriki na wawezeshaji wakifuatilia mada
Washiriki wa mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo wasimamizi wa rasilimali watu katika taasisi na Halamashauri mbalimbali nchini. Mafunzo hayo yanalenga kuwaweza waajiri hao kutafuta mbinu ikiwepo mafunzo na motisha mbalimbali kwaajili ya kuwafanya watumishi wapya wanapoajiriwa kuendelea kufanya kazi katika mazingira yeyote. 

No comments: