Advertisements

Saturday, June 18, 2016

Reggae Time ya Pride Fm June 18, 2016....Siku ya Mtoto wa Afrika

Katika kipindi cha wiki hii, niliungana na mwenzangu Kokuberwa Mushala kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika.
June 16, 1976 ni siku ambayo haitasaulika miongoni mwa wananchi weusi wa Afrika ya kusini. Ni siku ambayo watoto wa shule huko Soweto Afrika Kusini waliandamana kupinga elimu duni waliyokuwa wakipata na kutaka kukoma kwa ubaguzi. Maandamano hayo yalikutana na nguvu ya polisi makaburu ambao waliua watoto kwa risasi za moto.
Kwa wiki mbili mfululizo, maandamano ya watoto yaliendelea na zaidi ya watoto 100 waliuawa na maelfu kujeruhiwa.
Miaka 15 baadae, Umoja wa nchuru za Afrika OAU (kabla ya kuwa Umoja wa Afrika AU) ukaitangaza Juni 16 kuwa siku ya mtoto wa Afrika.

Kipindi cha REGGAE TIME kutoka Pride Fm Mtwara Tanzania hutayarishwa na kutangazwa na Mubelwa Bandio
Husikika kila Jumamosi kuanzia saa tisa kamili alasiri kwa saa za Afrika Mashariki
Radio hii yasikika duniani kote kupitia tovuti www.878pridefm.com na kwa walio Marekani na Canada wanaweza kuisikiliza kwa kupiga namba 832 280 0658
Ama kupitia TuneIn tun.in/seTTx

No comments: