Advertisements

Thursday, June 23, 2016

UBALOZI WA KUWAIT WATOA MSAADA WA MADAWATI 300

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye Hafla ya kukabidhi Madawati 300 kutoka Ubalozi wa Kuwait hapa nchini. Balozi Jasem Al Najem ndio aliyokabidhi msaada huo wa madawati. 
Juu na Chini ni sehemu ya Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakimsikiliza kwa Makini Waziri Mahiga alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo pichani) 
Balozi wa Kuwait nchini, Jasem Al Najem akizungumza katika hafla hiyo. 
Sehemu nyingine ya Wakuu Idara na Vitengo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 
Balozi Najem akiendelea kuzungumza 
Waziri Mahiga (kulia), Balozi Najem na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Abdallah Kilima, kwa pamoja wakiwa wamekaa kwenye madawati yaliyotolewa na Ubalozi wa Kuwait hapa nchini. 
Waziri Mahiga na Balozi Najem wakiwa katika picha ya pamoja na wakuu wa Idara na Vitego mara baada ya kumaliza mkutano na waandishi wa habari



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga ameupongeza Ubalozi wa Kuwait kwa kuwa wa kwanza kuitikia maombi yake ya kuchangia madawati kwa ajili ya shule za msingi na sekondari hapa nchini.
Pongezi hizo alizitoa jana wakati wa hafla ya kupokea madawati 50 kati ya 300 ambayo Ubalozi huo umeahidi kuipa Serikali. Hafla ilifanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
“Tumeanza kupokea madawati kutoka kwa rafiki zetu, huu ni mwanzo tu, na wengine watafuatia na taarifa ya kila dawati litakalokuwa linapatikana nitaiwasilisha kwa Mhe. Waziri Mkuu. Dkt. Mahiga alieleza.
Mhe. Waziri aliwaambia wahudhuriaji wa hafla hiyo kuwa katika utekelezaji wa malengo ya milennia, Tanzania ilifanya vizuri katika baadhi ya maeneo hususan, elimu na afya ya mama na mtoto. Licha ya idadi ya watoto kuandikishwa mashuleni iliongezeka, bado kulikuwa na changamoto ya kuboresha ubora wa elimu na upatikanaji wa vifaa vya kufundishia kama vile vitabu na majengo ya maabara na vifaa vyake.
Aliendelea kueleza kuwa baada ya Serikali ya awamu ya tano chini ya Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kutangaza elimu bure, udahili mashuleni umeongezeka maradufu na hivyo kusababisha changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba mkubwa wa madawati.
“Kufuatia hali hiyo, Serikali imejipanga kutumia mbinu mbalimbali kutatua changamoto hizo ikiwa ni pamoja na kuwaomba marafiki zetu watusaidie. Hivyo, Kuwait imejitokeza kutusaidia na imeahidi kusaidia sio madawati tu bali, hata maeneo mengine yenye changamoto kwenye elimu”.
Kwa upande wake, Balozi wa Kuwait, Mhe. Jasem Al Najem alisema kuwa msaada huo ni sehemu ya jitihada za Serikali yake kuunga mkono mkakati wa Rais Magufuli wa kutoa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 23 Juni 2016.

No comments: