Advertisements

Sunday, July 3, 2016

WATOTO WANAOLELEWA KATIKA KITUO CHA NEW HOPE FAMILY WAPATA MSAADA WA BAISKELI KWA AJILI YA USAFIRI WA SHULENI

Mkurugenzi Mkuu wa maduka ya woolworths nchini ,Joehans Mgimba akisalimiana na baadhi ya  Watoto wanaolelewa katika kituo cha New Hope Family Group, kilichopo Mwasonga Kata ya Kisarawe , Kigamboni jijini Dar es Salaam, wakati wafanyakazi wa Kampuni hiyo walipokwenda kutoa msaada wa Baiskeli na Vyakula mbalimbali kituoni hapo.Kulia ni mkuu wa fedha Samson Katemi.
Mkurugenzi Mkuu wa maduka ya Woolworths nchini, Joehans Mgimba akiwa amempakia kwenye baiskeli kijana Majaliwa Anthony, ambaye ni miongoni mwa Watoto wanaolelewa katika kituo cha New Hope Family Group Kilichopo Mwasonga Kata ya Kisarawe , Kigamboni jijini Dar es Salaam, ikiwa ni ishara ya kuonyesha jinsi watoto hao watakavyokuwa wanabebana wakati wa kwenda shule ili kuwahi masomo.kampuni hiyo ilitoa msaada wa baiskeri na vyakula mbalimbali kituoni hapo.
Watoto wanaolelewa katika kituo cha New Hope Family Group Kilichopo Mwasonga Kata ya Kisarawe , Kigamboni jijini Dar es Salaamwa wakiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Woolworths, mara baada ya kukabidhiwa msaada wa baiskeli na vyakula mbalimbali.  


No comments: