Advertisements

Sunday, July 10, 2016

WAZIRI MKUU WA ISRTAELI AFANYA ZIARA AFRIKA MASHARIKI

Waziri Mkuu wa Israeli, Benjamin Bibi Netanyahu, (katikati), akitabulishwa na mwenyeji wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Balozi Augustin Mahiga, (kushoto)na Rais wa Rwanda, Paul Kagame (kulia), Rais wa Zambia, Edgar Lungu na Waziri Mkuu wa Ethiopia
Hailemariam Desalegn, kwenye Ikulu ya Naklasero nchini Uganda.
Netanyahu akisalimiana na Balozi Mahiga
Netanyahu (kushoto0, na mwenyeji wake Waziri Mkuu wa Ethiopia,Hailemariam Desalegn
Netanyahu akiwa na Rais Museveni kwenye uwanja wa Entebe nchinihumo
Netanyahu akiweka shada la maua kwenye mnara huo wa kumbukumbu
Netanyahu akikagua gwaride la askari polisi nchini Kenya
Netanyahu akikagua gwaride uwanja wa ndege wa Entebe nchini Uganda
Netanyahu akiwa na Rais Uhuru Kenyatta, Ikulu ya Nairobi
Netanyahu akiteta jambo na mwenyeji wake, Rais wa Rwanda, Paul Kagame mjini Kigali
Kiongozi wa operesheni ya kuokoa mateka wa Israeli, Komandoo Yonatan Bibi Netanyahu. Kaka wa Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Bibi Netanyahu. Kiongozi huyo aliuawa kwenye harakati za 
kuokoa mateka


NA K-VIS MEDIA/NA MASHIRIKAYA HABARI

Waziri Mkuu wa Israeli, Benjamin Bibi Netanyahu, amekuwa ni kiongozi wa kwanza wa juu wa serikali ya nchi hiyo aliyeko madarakani kutembelea barani Afrika, tangu Yitzhak Rabin, aliyepata kuwa waziri Mkuu wan chi hiyo amtembelee Mfalme Hassan II wa Morocco, mnamo mwaka 1993.
Kituo cha kwanza cha Netanyahu kutembelea Afrika iliku Uganda, akaenda Kenya, na kumaliziana Ethiopia.
Akiwa Uganda, Netanyahu alifanya mkutano na baadhi ya viongozi wa nchi za Kiafrika kutoka Sudan Kusini, Tanzania, iliyowakilishwa na Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Kimataifa, Kikanda na Afrika Mashariki, Balozi Augustine Mahiga, na Zambia.
Hata hivyo pamoja na mkutano huo na viongozi wa kiafrika nchini Uganda, vyombo vya habari havikuutilia maanani zaidi mkutano huo na badala yake viliangazia zaidi tukio la kuzindua mnara wa kumbukumbu ya miaka 40 ya operesheni ya kijeshi iliyofanywa na Makomandoo wa Israeli wakati wakiokoa mateka raia wa Israeli kwenye uwanja wa ndege wa Entebe mnamo mwaka 1976.
Katika operesheni hiyo ya aina yake, kiongozi wa makomandoo hao, Yonatan Bibi Netanyahu, kaka wa Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu, aliuawa.
Israeli ililazimika kutuma makomandoo wake kuokoa raia wake waliotekwa nyara wakiwa ndani ya ndege ya shirika la ndegge la Ufaransa (Air France). Ndege hiyo ilitekwa nyara na wanamgambo wa Kipalestina, dakika 15 baada ya kuruka kutoka uwanja wa nege wa Tel-Aviv nchini Israel ikielekea Paris Ufaransa.
Wanamgambo hao wa Kipalestina, walifanya tukio hilo wakishinikiza wenzao waliokuwa wakizuiliwa kwenye magereZa nchini Israeli waachiliwe.
Tukio la kuuawa kwa Kakak wa Waziri Mkuu wa Israeli, ndio lililomsukuma kiongozi huyo kuingia kwenye siasa.
Hata hivyo mataifa mengi ya kiafrika hususan kusini mwa jangwa la Sahara, yalijuwa hayaiungi mkono Israeli kutokana na ukandamizaji wake dhidi ya Wapalestina.

Ukiacha Uganda, Netanyahu alikwenda Kenya, ambako enzi za utawala wa Kenyatta, Israeli ilikuwa swahiba wake, na hata 

No comments: