Advertisements

Friday, August 26, 2016

LUKUVI ATEMBELEA ENEO LA KILICHOKUWA KIWANDA CHA NGUO CHA KILITEX PUGU JIJINI DAR ES SALAAM

Mmoja ya Fundi gereji katika Mtaa wa Guluka Kwalala kata ya Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam Bw. Mohamed Ali akielezea sababu za wao kuvamia eneo la Kilichokuwa kiwanda cha nguo cha KiliTex kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi (hayupo pichani).
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimsikiliza kwa makini Afisa Ardhi toka Manispaa ya Ilala Bw. Furaha Mwakapalila akielezea historia ya eneo la Kilichokuwa kiwanda cha nguo cha KiliTex ambalo kwa sasa limevamiwa na mafundi magari wa kata ya Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam.
Afisa Tarafa wa Ukonga Bw. Jeremiah Makorere akifafanua jambo kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi wakati wa ziara ya waziri huyo kubaini migogoro mbalimbali ya ardhi katika eneo la Pugu Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Guluka Kwalala kata ya Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam ambao wamevamia eneo la Kilichokuwa kiwanda cha nguo cha KiliTex.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Guluka Kwalala kata ya Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam ambao wamevamia eneo la Kilichokuwa kiwanda cha nguo cha KiliTex.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Msimbazi kata ya Pugu Station jijini Dar es Salaam ambao wamevamia eneo la Kilichokuwa kiwanda cha matofali ya kuchoma cha Kisarawe Brick Factory (KIBRICO) wakati wa ziara ya Waziri huyo kubaini migogoro ya ardhi katika eneo la Pugu.
Mwenyekiti ya Kamati ya malalamiko ya wakazi wa Mtaa wa Msimbazi kata ya Pugu Station jijini Dar es Salaam ambao wamevamia eneo la Kilichokuwa kiwanda cha matofali ya kuchoma cha Kisarawe Brick Factory (KIBRICO) Bw. Deus King΄ung΄alo akisoma risala kwa niaba ya wakazi hao wakati wa ziara ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi wakati wa ziara ya Waziri huyo kubaini migogoro ya ardhi katika eneo la Pugu.

No comments: