Advertisements

Monday, August 22, 2016

MBUNGE AOMBWA KUVISAIDIA VITUO VYA AFYA JIJINI TANGA ILI KUIPUNGUZIA MZIGO HOSPITALI YA MKOA WA TANGA BOMBO

Mganga Mku wa Mkoa wa Tanga (RMO) Dkt Asha Mahita akisisitiza jambo wakati akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) ambaye alikwenda kuitembelea hospitali ya Mkoa wa Tanga Bombo kuangalia changamoto zinazowakabili
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Mussa Mbaruku akisisitiza jambo kwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga (RMO) Dkt Asha Mahita
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF) Mussa Mbaruku katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na madaktari kutoka katika taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya The Sunshine Muslim Volunteer huku wakishirikiana na madaktari bingwa kutoka nchi za Uingereza, Afrika kusini, Canada na Pakistani waliokuja kuweka kambi ya siku tano kwa ajili ya kutoa matibabu bure ya Fistula.
MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CUF), Mussa Mbaruku ameombwa kuangalia namna ya kuweka mkakati wa kuvisaidia vituo vya afya na Zahanati zilivyopo ndani ya Jiji la Tanga ili kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya mkoa wa Tanga Bombo inayohudumia wagonjwa wa mkoa mzima.

Ombi hilo lilitolewa jana na Mganga Mku wa Mkoa wa Tanga (RMO) Asha Mahita wakati Mbunge huyo alipoitembelea hospitali ya alisema kuwa msongamano unaoikabili Hospitali ya Rufaa ya Mkoa unatokana na kutokuwepo na ubora katika zahanati na vituo vya afya jambo ambalo linalowafanya wanachi kukimbilia katika Hosptiali hiyo.

Hatua hiyo inatokana na zahanati na vituo vya afya vingi Jijini Tanga kukakabiliwa na changamito nyingi zinazo sababisha kukosa ubora hali inayochangia kwa asilimia kubwa wananchi wengi kukimbilia katika hospital ya Rufaa ya Bombo na kuongeza msongamano wa wagonjwa.

Mahita alisema ipo haja ya kuvisaidia vituo hivyo ambavyo havina nyumba za watumishi, uzio, miundombinu mibovu na vingine kukosa umeme jambo ambalo linakuwa si rafiki kwa wahudumu na linakwamisha shughuli za kiafya hasa nyakati za usiku.

Alisema kuwa iwapo kutakuwepo na mabororesho katika vituo hivyo huku Serikali na wadau mbalimbali wakiweka nguvu zao katika swala la kumalizia Hospitali ya wilaya ambayo mpaka sasa inajengo moja la ghorofa kwa ajili ya utawala ikimaliziwa na kuanza kutumika kutapunguza kwa asilimia kubwa msongamano kwenye hospitali hiyo.

Kwa upande wake, Mbunge Mussa Mbaruku alihaidia kuangalia namna ya kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo kwani wananchi afya zao zinapokuwa zimeimarika inawasaidia kuweza kufanya shughuli za kujiingizia kipato.

“Ndugu zangu huu si muda wa kupiga porojo kuhusiana na masuala ya afya ambalo ndio uti wa mgongo wa wananchi hivyo lazima viongozi wajenge umoja na kutafuta njia ya kuweza kuviboresha vituo hivyo ambavyo vitawasaidia kwa asilimia kubwa wananchi kupata huduma hiyo kwa ukaribu zaidi “Alisema

Aidha alisema pamoja na changamoto zinazozikabili zahanati na vituo hivyo lazima Serikali itenge fedha za kutosha ili kuweza kuimalizia Hospitali ya Wilaya iliyopo Masiwani Shamba ambayo mpaka sasa bado hakuna majibu sahihi ya kukwama kwa umaliziwaji wa Hosptili hiyo.

“Bado nashindwa kupa majibu ni kitu gani kinachokwamisha kumalizika kwa Hospitali ya Wilaya ambayo tayari inajengo zuri la utawala tena la ghorofa serikali inawajibu kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha Hospitali hiyo inamalizika na inakuwa na kiwango bora katika sekta zote za matibabu.

Mbaruku alifanya mazungumzo hayo na mganga mkuu wa Mkoa alipo watembelea madaktari kutoka katika taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya The Sunshine Muslim Volunteer huku wakishirikiana na madaktari bingwa kutoka nchi za Uingereza, Afrika kusini, Canada na Pakistani waliokuja kuweka kambi ya siku tano kwa ajili ya kutoa matibabu bure ya Fistula.

Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

No comments: