Na Yeremias Ngerangera-Namtumbo
Mtoto Zawadi Hasani (14) wa
kitongoji cha Majengo katika kijiji cha Mkongo wilayani Namtumbo
Mkoani Ruvuma amejinyonga kwa kutumia chandarua chake akiwa chumbani
kwake baada ya kuchoshwa na kauli zisizo na staha kutoka kwa mama
yake.
Tukio hilo limetokea hivi karibuni
,ambapo mwili wa marehemu ulikutwa chumbani kwake asubuhi siku ya
ijumaa baada ya mama yake mzazi kumtaka aamke na ndipo jitihada zake
za kumtaka aamke kwa kumwita mlangoni zilipogonga mwamba aliamua
kufungua mlango na kuukuta mwili wa mwanae ukiwa juu ukining’inia.
Mtendaji wa kata ya Mkongo Whclif
Mlinda alifika katika eneo la tukio na kuthibitisha kifo cha kijana
huyo kilichosababishwa na kujinyonga kwa kutumia chandarua kutokana
na kauli zisizo na staha kutoka kwa mama yake mzazi huyo
marehemu.
Kwa mujibu wa bwana Mtinda amesema
kuwa kabla ya kwenda kulala marehemu alikuwa anadai hela yake kutoka
kwa mama yake ambazo alimpa mama yake huyo amwekee na alipozihitaji
kuzichukua kauli zisizo na staha zilitolewa na mama huyo kwa mwanae
na kuibuka sintofahamu kati yao.
Malumbano ya mama huyo na mwanae
yaliendelea usiku huo hatua iliyofikia mama huyo kumtaka mwanae
aondoke na aende akaishi na baba yake mzazi kwa kuwa baba ya
marehemu na mama huyo waliachana na marehemu aliamua kwenda kuishi na
mama yake huyo.
Aidha kitendo cha mama huyo
kumweleza mtoto wake aende akaishi kwa baba yake na kumnyima fedha
yake aliyoiweka kwake ndicho kilichomkasirisha kijana huyo na kisha
kuamua kujinyonga alisema bwana Mtinda.
Marehemu amezikwa kijiji cha Mkongo
na kumwacha mama yake katika hali ya kutoamini kilichotokea kwa madai
kuwa uamuzi aliouchukua mwanae wa kujinyonga unamwumiza moyoni na
utaendelea kumwumiza moyoni alisema mama huyo.
No comments:
Post a Comment