Advertisements

Tuesday, August 16, 2016

OFISI YA SERIKALI YA MTAA WA MWEMBENI MANZESE YAGEUZWA SEHEMU YA KUTUPA TAKA

Mkazi wa Mtaa wa Mwembeni Manzese jijini Dar es Salaam, Rajabu Kassim akitupa taka nje ya Ofisi ya Serikali ya Mtaa baada ya gari la kuzoa taka katika mtaa huo kushindwa kupita kwa wakati na kusababisha mlundikano wa taka majumbani.
Mkazi wa Mtaa wa Mwembeni Manzese jijini Dar es Salaam akitupa taka mbele ya Ofisi ya Serikali ya Mtaa na kusababisha ofisi nzima kutoa harufu kali.(Picha na Francis Dande)


NA FRANCIS DANDE
WANANCHI wa mtaa wa Mwembeni Kata ya Manzese jijini Dar es Salaam wameibua taharuki baada ya kwenda kutupa uchafu ‘Taka taka’ kwenye Ofisi ya Serikali ya Mtaa wa Mwembeni.

Uamuzi ulitokana na madai ya wananchi hao kwamba ofisi hiyo imeshindwa kutekeleza utaratibu wa kuzoa taka kwenye maeneo hayo takribani kwa miezi mitatu.

Wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo baadhi ya wananchi hao walibainisha kuwa wamekuwa wakitozwa ushuru wa kuzolewa uchafu kila mara lakini hakuna gari lililokuwa likizo taka hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisi hapo, Ofisa Mtendaji wa Kata hiyo, Fatuma Abdallah ambaye akutaka kupigwa picha alikiri kwamba ni kweli tatizo la kuchukua taka limekuwa sugu mtaani hapo.

Alisema hapendi kuona uchafu ukikithiri hadi kufikia hatua ya wananchi kumfikishia taka ofisi kwake lakini imewaradhimu kutokana na mfumo uliopita ulikuwa mbovu katika usimamizi.

“Mimi ni mgeni hapa, nina miezi mitatu tangu nianze kazi na nimekuta kuna deni la ubebaji taka jambo ambalo limenipa wakati mgumu katika kusimamia uzoa wa uchafu kwa muda muhafaka,” alisema.

Mjumbe wa Shina namba 57, Zainab Abdalah amesema kuwa kutokana na kero ya uchafu uliorundikana majumbani kwao wameamua kuja kuzileta katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa ili kuushinikiza uongozi wa Kata hiyo kuziondoa taka hizo zilizorundikana majumbani kwao.

Naye Mkazi wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina la Odo Said alisema kuwa wamekuwa wakichangishwa kiasi cha shilingi 2000 kwa mwezi kwa ajili ya kupata huduma ya kuzolewa taka lakini hata wanapofanya hivo magari yamekuwa hayafiki kwa wakati na kusababisha mrundikano wa taka nyingi majumbani na hivyo kuhatarisha afya zao kutokana na kuhofia kupata magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu.

CHANZO: HABARI MSETO BLOG

No comments: