Advertisements

Friday, September 23, 2016

MWALIMU AHUKUMIWA MIAKA MITATU JELA KWA KUOMBA RUSHWA YA SH. 130,000

Mahakama  ya Hakimu Mkazi ya Bukombe mkoani Geita imemhukumu Mwalimu wa Shule ya Msingi Umoja, Daniel Nyingati kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya Sh milioni 1.6 baada ya kupatikana na makosa ya  kuomba na kupokea rushwa.

Hukumu hiyo ilitolewa juzi na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Bukombe, Gabriel Kurwijila.

Alisema  mshitakiwa Nyingati amekutwa  na hatia ya kuomba  rushwa ya  Sh 130,000 kutoka kwa Marco Elias  aweze kumdahili mtoto wake aliyekuwa amehitimu  masomo ya shule ya msingi kinyume na sheria.
Hakimu Kurwijila alisema   ushahidi ulitolewa mahakamani pande zote mbele ya  waendesha mashitaka kutoka  Taasisi ya Kuzuia na Kudhibiti Rushwa Tanzania (Takukuru), Kelvin Murusuri na  Husna Kiboko umejitosheleza na kumtia hatiani mwalimu Nyingati.

Alisema mahakama inamhukumu mwalimu Nyingati kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya Sh milioni 1.6 kwa kuwa alitenda kosa la kuomba na kupokea rushwa.

No comments: