Advertisements

Monday, October 3, 2016

BENKI YA NMB TAWI LA MLIMANI CITY JIJINI DAR ES SALAAM YAZINDUA HUDUMA KWA WATEJA ILIYOZINDULIWA NA BENKI HIYO DUNIANI KOTE LEO

 Muweka Hazina wa Benki ya NMB, Aziz Chacha (wa pili kulia), akizungumza  na wafanyakazi wa Benki hiyo na wateja wakati wa hafla ya uzindua wa wiki ya Huduma kwa wateja Duniani kwa benki hiyo uliofanyika Tawi la Mlimani City Dar es Salaam leo asubuhi. Kulia ni Meneja wa Tawi hilo, Seka Urio. 

  Muweka Hazina wa Benki ya NMB, Aziz Chacha (kushoto), akimkabidhi zawadi Amani Mgweno ya kuwa mfanyakazi bora wa benki hiyo tawi la Mlimani City kuanzia mwezi Januari hadi Oktoba.

 Mkuu wa Kitengo cha Uajiri wa benki hiyo, Mbonny Maumba akisalimiana na wateja katika hafla hiyo ya uzinduzi.
 Hapa wafanyakazi wa benki hiyo wakitakiana heri na wateja.
 Ni furaha tupu katika uzinduzi huo.
 Hakika wamependeza meno yote nje kwa furaha ya uzinduzi huo ambao ni muhimu kwa benki hiyo.

 Uzinduzi ulikwenda sanjari na maakuli.
 Hapa ni chai na mahojiano na waterja wa benki hiyo.
 Mteja wa benki hiyo, Regina Cyrillo akitoa maelezo ya huduma bora zinazotolewa na benki hiyo.
 Mdau wa benki hiyo, Novatus Shiyo akitoa maelezo jinsi wanavyotufaika na huduma za benki hiyo. Wengine ni wateja wa benki hiyo tawi la Mlimani City.
 Mhandisi Heriel Muhulo ambaye ni Ofisa Mtendaji wa Kampuni ya Ujenzi ya Hematec Inn Ltd ya Sinza jijini Dar es Salaam akielezea mafanikio wanayopata kwa kuwa wateja wa benki hiyo.
 Mdau wa benki hiyo kutoka kampuni ya Binaisa Ltd, Mr Mapunda akitoa maelezo yake kuhusu benki hiyo.
 Meneja wa benki hiyo tawi la Mlimani City, Seka Urio (kulia), akizungumza kwenye hafla hiyo.
 Viongozi na baadhi wafanyakazi wa benki hiyo wakifurahia uznduzi huo.


Picha ya pamoja viongozi wa benki hiyo wafanyakazi pamoja na wateja katika hafla hiyo.

No comments: