Advertisements

Saturday, October 1, 2016

JOZI LOUNGE YADHAMINI MISS TANZANIA 2016

Washiriki wa shindano la Miss Tanzania 2016 wakiwa katika moja ya pozi jana mara baada ya kuwasili Jozi Lounge, ambapo watakuwa hapo kwa siku tatu mfululizo. Jozi lounge ni mojawapo wa wadhamini wa mashindano ya miss tanzania mwaka huu 2016
 Wakipata vinywaji kwa pamoja huku wakifurahia utulivu mwanana ndani ya Jozi Club
Baadhi ya Washiriki wa shindano la Miss Tanzania 2016,ambapo jana wameingia kambini pia walipata muda wa kuserebuka ndani ya Club maarufu kwa jina la Jozi Lounge iliopo msasani jiji Dar EsSalaam.

 Washiriki wa Miss Tanzania 2016 wakiserubuka ndani ya Jozi Club kwa raha zao
Club maarufu kwa jina la Jozi Lounge iliopo msasani jijini Dar Es Salaam, imejitokeza hivi karibuni kujiunga na moja katika kampuni na taasisi zilizokwisha kujitokeza kudhamini zoezi zima la kutafuta mrembo wa tanzania atakayepeperusha na kuitangaza Tanzania katika anga za kimataifa katika Nyanja mbalimbali yakiwemo utalii na huduma ya jamii yenye mahitaji maalum.

Akizungumza na warembo kutoka mikoa yote Tanzania ambao wanatarajia kuchuana vikali mwishoni mwa mwezi wa kumi huko jijini Mwanza na hatimaye kumpata mshindi wa Miss Tanzania 2016, Mkurugenzi wa Jozi Lounge Bw.Dismas Massawe amesema Jozi Lounge itawadhamini warembo hao kwa kuwapatia malazi, chakula na mahitaji mengine muhimu kwa kipindi cha siku tatu ambapo jana ilikuwa uzinduzi na leo ni siku ya semina mbalimbali na siku ya jumapili itakuwa siku ya kusherehekea ushindi wa mikoa tayari kuelekea katika mapambano ya ngazi ya Taifa.

No comments: