Advertisements

Monday, October 17, 2016

MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MKINGA TANGA MBARONI KWA KUMTISHIA BASTOLA ASKARI WA USALAMA BARABARANI

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkinga Tanga Emmanuel Barnabas Mkumbo, anashikiliwa na Polisi Morogoro kwa kujifanya usalama wa Taifa na kumtishia Bastola askari wa usalama barabarani.
Jeshi la Polisi mkoani Morogoro inamshikilia Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mkinga mkoani Tanga Emmanuel Barnabas Mkumbo baada ya kujifanya usalama wa Taifa nakumtishia kwa Bastola askari wa usalama barabarani wakati wakielekea kituo kidogo cha polisi Kingoluwira, alikotaka apelekwe kuzungumza na mkuu wa kituo baada ya kukamatwa akiwa amezidisha Mwendo kasi (SPEED) barabara kuu ya Morogoro - Dar es Salaam.

Chanzo: ITV

No comments: