Advertisements

Friday, November 25, 2016

MAKONDA ATIKISA UBUNGO, AMKARIBISHA RAIS MAGUFULI KUZUNGUMZA LIVE KWA SIMU KWENYE MKUTANO WA HADHARA ENEO LA MARAMBA MAWILI LEO

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akikata utepe kuzindua vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari ya Urafiki wilayani Ubungo mkoani humo, leo akiwa katika ziara kukagua utekelezaji wa Ilani ya Chama, kusikiliza kero za wananchi na kujadili nao namna ya kuzitatua. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Humphrey Polepole.
Makonda akiondoka baada ya kuzindua vymba hivyo vya madarasa katika shule ya sekondari ya Urafiki
Makonda akimtania mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Urafiki Rajabu Fadhili, baada ya kuzindua vyumba vya madarasa kwenye shule hiyo leo
Makonda akimtania mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Urafiki Rajabu Fadhili, baada ya kuzindua vyumba vya madarasa kwenye shule hiyo leo
Makonda akimtania mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Urafiki Rajabu Fadhili, baada ya kuzindua vyumba vya madarasa kwenye shule hiyo leo

Makonda akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Ubingo Humphrey Polepole, baada ya kuzindua vyumba vya madarasa kwenye shule hiyo leo
Wananfunzi wakisubiri kumsikiliza Makonda baada ya kuzindua vyumba vya madarasa ya shule hiyo leo
Mkuu wa wilaya ya Ubungo Polepole akizungumza maneno ya utangulizi kumkaribisha makonda kuzungumza.

MAKONDA AKIFURAHIWA NA WANANFUNZI WAKATI AKIONDOKA BAADA YA KUZINDUA VYUMBA VYA MADARASA

MKUTANO WA HADHARA MARAMBA MAWILI
Wananchi wa King'zanzi, Malamba mawili, wakiwa na bango lenye ujumbe waliokusudia aupate Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alipohutubia mkutano wa hadhara kusikiliza kero za wananchi katika eneo hilo leo
Mwananchi akiluiza swali kuhusu kero ya vijiwe vya wavutabangi na vibaka ambao alidai wamekuwa wakikamatwa na polisi na kisha kuachwa.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akijibu baadhi ya maswali kwa kuwaita wahusika kutoka katika maofisa kadhaa alipofuatana nao katika msafara wake akiwemo kutoka sekta mbalimbali ili kujibu hoja za wananchi. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida
Mwananchi akiluiza swali kuhusu mgogoro wa ardhi katika eneo la Malamba Mawili, wilayani Ubungo. Mkuu wa mkoa Paul Makonda pamoja na kutoa majibu kwa kuwataka wahusika kutoa maelezo, pia alimwalika Rais Dk John Magufuli kuzungumzoa masuala ya migogoro ya ardhi hasa kwa wanaopakana na barabara kuu katika eneo la Ubungo. Kulia ni Ofisa kutoka TANROADS ambaye hata hovyo hakuweza kutoa majibu kama ilivyotarajiwa na badala yake muulizaji alipewa ufafanuzi wa kina na Mkuu wa wilaya ya Ubungo Humphrey Polepole.
Wananchi wakiwa wametulia wakati Rais Dk John Magufuli alipokuwa akitoa majibu kwa njia ya simu, kuhusu migogoro ya ardhi kwa wanaopakana na barabara kuu katika eneo la Ubungo
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Humphrey Polepole akifunga mkutano. Kushoto ni Mkuu wa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam. Paul Makonda. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO- theNkoromo Blog

No comments: