Advertisements

Saturday, November 26, 2016

VIJANA WAIOMBA SERIKALI KUENDELEA NA MCHAKATO WA KATIBA MPYA

Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Bw. Hebron Mwakagenda akitoa mafunzo kuhusu katiba ya zamani pamoja na katiba mpya kwa vijana kutoka wilaya zote za jiji la Dar es Salaam leo. (Picha na Geofrey Adroph)
Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania Bw, Deus Kibamba akitoa elimu kuhusu mchakato wa mabadiliko ya Katiba pamoja na historia ya mchakato huo kwa vijana wa  wilaya zote za jiji la Dar Es Salaam.
Katibu Mtendaji wa TYVA, Saddam Khalfan akitoa ufafanuzi kuhusu shirika hilo na madhumuni ya mjadala wa katiba na vijana uliyofanyika katika ukumbi wa Blue Pearl jijini Dar Es Salaam

Mbunge wa Viti Maalumu, (CUF), Riziki Lulida akizungumzia changamoto wanazozipata kama wabunge wenye ulemavi katika katiba pamoja na kutoa maoni kuhusu uundwaji wa katiba mpya
Mbunge wa Viti maalum Pemba-Zanzibar, Mheshimiwa Zainabu Mussa Bakari akizungumzia Haki na Wajibu wa mwananchi Kikatiba wakati wa ufunguzi wa Kongamano lililowashirikisha vijana mbalimbali kutoka wilaya tano za jiji la Dar es Salaam ili kujadili katiba mpya lililoandaliwa na Taasisi ya Vijana ya TYVA pamoja na IRI.
Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Dar es salaam Salma Mwasa (CUF) akizungumza na vijana kuhusu balaza la vijana katika katiba inayopendekezwa ili kuweza kuleta utatuzi wa matatizo tyao ili serikali iwasikie wakati wa kongamano lililowakutanisha vijana kutoka katika wilaya mbalimbali za jiji la Dar.
Baadhi ya vijana wakichangia mada
Baadhi ya Vijana wa wilaya ya mbalimbali za jijini Dar es Salaam wakiwa kwenye mafunzo kuhusu mchakato wa mabadiliko ya Katiba yaliyofanyika leo ambao wameazimia kuendelea kwa mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya.

No comments: