Advertisements

Thursday, December 1, 2016

SEMINA YA MAFUNZO KWA WARATIBU WA MADAWATI YA UWEZESHAJI WA MIKOA YOTE YA KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI YAFANA

Naibu Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Bw. Constantine Mushi akisisitiza jambo wakati wa ufunguzi  wa semina ya mafunzo kwa waratibu wa madawati ya uwezeshaji wa kanda ya nyanda za juu kusini juu ya uwakirishi wa wananchi katika uwekezaji. Kushoto ni Afisa mkuu wa manunuzi wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Bw..Adangson Mwaigomole. wapili kushoto ni Afisa Uwezeshaji Mkuu wa NEEC, Bw. Oswadi Karadisi. kulia ni Katibu Tawala Msaidizi - Uchumi na Uzalishaji Mkoani Mbeya, Bw.Nyasebwa Chimagu.
Afisa Uwezeshaji Mkuu(LOCAL CONTENT) wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bw. Oswadi Karadisi.akitoa mada kwenye semina ya mafunzo kwa waratibu wa madawati ya uwezeshaji wa mikoa yote ya kanda ya nyanda za juu kusini juu ya ushiriki wa wananchi katika Uwekezaji(Local Content). Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Mbeya na kuratibiwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Waratibu wa madawati ya uwezeshaji kutoka kanda ya nyanda za juu kusini wakifatilia mada toka kwa mwezeshaji katika semina ya mafunzo ya ushiriki wa wananchi katika uwekezaji (Local Content). Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Mbeya na kuratibiwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Naibu Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya Bw. Constantine Mushi akifurahi jambo na Afisa Mkuu wa Manunuzi wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi( NEEC) Bw.Adangson Mwaigomole mara baada ya kufungua semina ya siku mbili ya mafunzo kwa waratibu wa madawati ya uwezeshaji wa kanda ya nyanda za juu kusini juu ya uwakirishi wa wananchi katika uwekezaji (Local Content).kushoto ni Afisa Uwezeshaji Mkuu-Local Content wa NEEC, Bw. Oswadi Karadisi.

No comments: