Advertisements

Wednesday, January 11, 2017

MKURUGENZI TAASISI YA ILTC YA JIJINI MWANZA AOMBA SERIKALI KUZISAIDIA TAASISI BINAFSI ELIMU.

Na George Binagi-GB Pazzo
Taasisi ya lugha ya International Language Traing Centre iliyopo Isamilo Jijini Mwanza, imeiomba serikali kuzisaidia taasisi binafsi za kelimu nchini ili kutimiza vyema wajibu wake.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Mwalimu Charles Mombeki (pichani), ameyasema hayo wakati akizungumza na Lake Fm ya Mwanza na kuomgeza kwamba ikiwa serikali itafanya hiyo, itazisaidia taasisi hizo kutekeleza vyema wajibu wa kutoa elimu bora kwa wananchi.

Amesema si vyema serikali kuzifungia taasisi binafsi za kielimu ikiwemo shule na vyuo pindi zinapokabiriwa na changamoto za kielimu badala yake inaweza kuzisaidia katika kuondokana na changamoto hizo.

Taasisi ya International Language Training Centre inajihusisha na uendelezaji wa lugha mbalimbali ikiwemo lugha za asili, Kiswahili, kiingereza, kifaransa na nyinginezo.
Bonyeza hapa kusoma zaidi

No comments: