Advertisements

Monday, May 8, 2017

NAIBU MEYA WA MANISPAA YA ILALA AKABIZI JEZI NA MASHINE YA KUONSHEA GARI


Na Mwandishi wetu,Tz

NAIBU Meya wa Manispaa ya Ilala ambae pia ni Diwani wa kata ya Vingunguti Omar Kumbilamoto amewataka Madiwani na wenyeviti wa Serikali za mitaa (CUF) kufanya kazi kwa bidii na kutoyumbishwa na mgogoro uliopo ndani ya chama hicho ili kuleta maendeleo kwa wananchi wao.

Pia amesema mgogoro huo ni mdogo sana ndani ya chama hivyo,ni vyema kuelekeza juhudi zao katika kuwasaidia wananchi kuwatatulia changamoto zao ambazo wamekua wakikabiliana ndani ya jamii.

Rai hiyo aliitoa jijini Dar es Salaam jana wakati alipokua akitoa msaada kwa wananchi wa kata hiyo ikiwemo mashine ya kuoshea gari pamoja na jezi za michezo wenye thamani ya sh.mill.1.2 lengo ikiwa lengo ni kuleta mabadiliko ya haraka kwa wananchi hao.

Kumbilamoto alisema,licha ya mafanikio yaliopatikana kwa kipindi kifupi lakini pia wanakabiliwa na changamoto ya bati zaidi ya 1300 kwa ajili ya kuezekea shule zote zilizopo katika kata hiyo ambapo amemuomba Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali (TAMISEMI) Goerge Simbachawene kuwatafutia wadau wa kuweza kuwasaidia

"Tatizo la uchakavu wa majengo ndani ya kata yangu imekua ni tatizo kubwa hususani kipindi hichi cha mvua kwani wanafunzi hulazimika kuhamishiwa madarasa , na ukiangalia pesa za kodi ya majengo ambazo tunazipata sisi kama Manispaa ni kidogo zote zinaenda Serikali kuu"alisema Kumbilamoto.

Aidha aliongeza kuwa,kwa upande wa ukarabati wa barabara ya Mnyamani Vingunguti iliopo Manispaa ya Ilala, suala hilo lipo katika hatua ya mwisho kwani wanasubiri idhini ya mkuu wa mkoa kuweza kuruhusiwa mkandarasi kuanza kazi mara moja.

"Sisi kama Manispaa ya Ilala tuna uwezo wa kumruhusu mkandarasi huyu lakini awali mkuu wa mkoa aliwafungia wakandarasi watatu kutokujenga barabara yoyote ndani ya mkoa wake ambapo na huyu ni miongoni mwa waliofungiwa,"alisema Kumbilamoto..

No comments: