Advertisements

Sunday, June 18, 2017

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala (wa tano kushoto) akipokea karatasi yenye orodha ya Vifaa vya kutolea huduma za Afya kutoka kwa Mbunge wa Kibaha Mjini, Silyvestry Koka (kushoto kwake) wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa hivyo vyenye thamani zaidi ya Sh. milioni 400 iliyofanyika kwenye Kituo cha Afya Mkoani, mjini Kibaha, leo mchana. Kulia kwa Waziri ni MKuu wa Wilaya ya Kibaha, Asumta Mshama. Picha Zote na Muhidin Sufiani (MAFOTO).
Makabidhiano yakiendelea......
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala, akikagua sehemu ya vifaa hivyo wakati akikabidhiwa na Mbunge wa Kibaha Mjini, Silyvestry Koka (kulia kwake).
Mbunge wa Kibaha mjini, Silyvestry Koka, akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi Vifaa vya kutolea huduma za Afya, iliyofanyika kwenye Kituo cha Afya cha Mkoani mjini Kibaha. Kushoto kwake ni Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mjini, Asumta Mshama.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mbunge Koka, alisema kuwa alifanikiwa kupata msaada wa vifaa hivyo kutoka kwa rafiki zake waishio nchini Marekani, wakati alipokwenda katika shughuli zake za kibiashara, ambapo walimhakikishia kupata vifaa hivyo kwa kuchangia gharama za usafirishaji hadi kuingia nchini.

Baada ya uhakika huo Koke alitumia gharama zake kuwasafirisha baadhi ya wataalamu (Wazungu) kutoka nchini Marekani na kuja nchini hadi Mji wa Kibaha kwa lengo la kukagua na kujiridhisha juu ya uhitaji wa vifaa hivyo vya kutolea huduma za afya, ambapo alitumia jumla ya Sh. milioni 12.

Aidha alisema kuwa vifaa hivyo vilichelewa kutokana na uhitaji kutoka mataifa mengine yaliyokuwa yakipata matatizo na magonjwa ya mlipuko, na hivyo kampuni hiyo ya Project Cure, kulazimika kughairisha kusafirisha kuja nchini na kutoa kipaumbele kwa mataifa hayo yaliyokuwa yakipata matatizo kwanza.

Mbali na Mbunge kuchangia kiasi cha Sh. milioni 12, pia Halmashauri ya Mji wa Kibaha pia ilichangia kiasi cha Sh milioni 32, zilizosaidia kusafirisha vifaa hivyo kutoka nchini Marekani hadi kuwasili nchini. Vifaa hivyo vilivyokabidhiwa hii leo vina thamani ya zaidi ya Sh. milioni 400.
Sehemu ya vifaa hivyo.......
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala, Mbunge wa Kibaha Mjini, Silyvestry Koka, wakitoka kutembelea katika Wodi ya Wazazi, katika Kituo cha Afya Mkoani, leo mchana wakati alipofika kukabidhi Vifaa vya kutolea huduma za Afya vyenye thamani ya zaidi ya Sh.milioni 400. 
NAIBU Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala, (kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mfanyakazi wa Chumba cha Maabala cha Kituo cha Afya Mkoani, Farida Chagulaga, wakati waziri huyo alipotembelea chumba hicho na kukagua taratibu za ufanyaji kazi, alipofika kwa ajili ya kukabidhi vifaa vya kutolea huduma za afya.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala, (katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mfanyakazi wa Chumba cha Maabala cha Kituo cha Afya Mkoani, Farida Chagulaga, wakati waziri huyo alipotembelea chumba hicho na kukagua taratibu za ufanyaji kazi, alipofika kwa ajili ya kukabidhi vifaa vya kutolea huduma za afya.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala (wa pili kushoto) Mbunge wa Kibaha Mjini, Silyvestry Koka (kushoto kwake) Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Asumta Mshama (kushoto) wakikabidhi karatasi ya orodha ya vifaa vya kuhudumia wagonjwa kwa Madaktari wa Kituo cha Afya cha Mkoani mjini Kibaha, wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo vyenye thamani ya zaidi ya Sh. Milioni 400.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala (wa tatu kulia) Mbunge wa Kibaha Mjini, Silyvestry Koka (kulia kwake) Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Asumta Mshama (wa pili kulia) na baadhi ya waganga wa Kituo cha Afya cha Mkoani Kibaha, wakikagua badhi ya Vitanda vya wagonjwa, baada ya makabidhiano ya vifaa hivyo vya kutolea huduma kwa wagonjwa vyenye thamani zaidi ya Sh. milioni 400. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye Kituo cha Afya Mkoani, mjini Kibaha.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala, akiimba wimbo maalumu kwa pamoja na Mkuu wa Wilaya Asumta Mshama (kulia), Mbunge wa Kibaha mjini, Silyvestry Koka, alipokuwa akizungumza na wananchi wa mji wa Kibaha, Wafanyakazi wa Kituo cha Afya cha Mkoani (hawapo pichani) wakati wa hafla ya makabidhiano ya Vifaa vya kutolea huduma za afya kituoni hapo
Dkt. Kigwangala, akizungumza wakati wa hafla hiyo.....
Baadhi ya wananchi wakimsangilia mgeni rasmi wakati akitoa hotuba yake katika hafla hiyo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wananchi wa mji wa Kibaha baada ya hafla hiyo. 
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala, akiagana na baadhi ya wanachi waliohudhuria hafla hiyo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala, akiagana na baadhi ya wanachi waliohudhuria hafla hiyo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala, akiagana na baadhi ya wanachi waliohudhuria hafla hiyo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Hamis Kigwangala, akiagana na Diwani Selina.
Wasanii wa Kikundi cha Malaika Dance, cha Kibaha wakitoa burudani katika hafla hiyo

No comments: