Advertisements

Sunday, August 13, 2017

CHAMA CHA AFYA YA JAMII TANZANIA CHATANGAZA MKUTANO WAKE MKUU WA 34 WA MWAKA

Na Dotto Mwaibale

Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA) kimetangaza mkutano wa mkuu wa 34 wa mwaka ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni Sera za Afya kwanza katika utekelezaji wa malengo 17 ya Maendeleo endelevu 2016-2030.

Wadau wa maendeleo hasa idara za  Serikali, Sekta Binafsi, Vyuo Vikuu, Taasisi za Utafiti na Mashirika yasio ya kiserikali na ya kimataifa na wananchi kwa ujumla wameombwa kuwakilisha andiko litakalosomwa kwenye mkutano huo na kisha kujadiliwa na hata kufikia maazimio ya pamoja mkutano huo kwa mwaka huu unatarajia kufanyika mkoani Singida.




No comments: