Advertisements

Friday, August 25, 2017

TANZIA

C:\Users\malaler.FOREIGN\Desktop\Marehemu Mzee Paul Joseph Maro.jpg
Marehemu Mzee Paul Joseph Maro
14.03.1931 - 23.08.2017
Familia ya Mzee Paul Joseph Maro ya Dar es Salaam inasikitika kutangaza kifo cha Baba yao Mpendwa Mzee Paul Joseph Maro kilichotokea katika hospitali ya Muhimbili juzi alfajiri Jumatano tarehe 23.08.2017.
Marehemu Mzee Paul Joseph Maro ni baba mzazi wa:
1. Happiness Paul Maro
2. Gabriel Paul Maro
3. Edwin Paul Maro na
4. Simon Paul Maro
Maandalizi ya Mazishi yanafanyika nyumbani kwa marehemu Tandika Maghorofani karibu na Chuo cha Bandari.
Habari ziwafikie ukoo wote wa Maro , Mawalla, Marealle na Mandara, ndugu jamaa na marafiki wote wa familia.
Mazishi yatakuwa kesho Jumamosi tarehe 26.08.2017 katika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.
Ratiba itaanza saa tatu asubuhi nyumbani kwa marehemu ambapo shughuli ya kutoa heshima za mwisho kwa marehmu itafanyika.
Saa saba misa ya kumuombea marehemu itafanyika katika kanisa la katoliki Chang'ombe ambapo pia itaambatana na kutoa heshima za mwisho.
Mida ya saa tisa safari ya kuelekea kwenye makaburi ya  Kinondoni itaanza.

“Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, imani nimeilinda"
2 Timotheo 4:7

No comments: