Advertisements

Monday, September 25, 2017

DC MTATURU ASIFU UTENDAJI WA MBUNGE ELIBARIKI KINGU

Mbunge wa Jimbo La Singida Magharibi Mhe Elibariki Kingu akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi ulioketi kuchagua viongozi wapya watakaoiongoza jumuiya hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu (Mwenye shati la Njano), Mbunge wa Jimbo la Singida Mgharibi Mhe Elibariki Kingu (Wa Kwanza kushoto Pichani) na viongozi wengine wakifatilia Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana Wilaya ya Ikungi katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Ikungi.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya Siasa Wilaya akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi ulioketi kuchagua uongozi wapya watakaoiongoza jumuiya hiyo.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi wakimsikiliza mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano huo Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu kabla ya kuchagua uongozi wapya kuongoza jumuiya hiyo ngazi ya Wilaya.

Na Mathias Canal, Singida


Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi Mhe Elibariki Kingu ametajwa kama Kiongozi makini anayejali maslahi ya wananchi wa Jimbo, Wilaya, Mkoa na Taifa kwa ujumla katika kipindi kifupi cha utendaji wake tangu alipochaguliwa na wananchi Octoba 25, 2015.

Heko hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakati akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Ikungi kwenye mkutano ambao ajenda yake kubwa ni uchaguzi wa uongozi wa jumuiya hiyo ngazi ya Wilaya.

Mbele ya wajumbe hao katika Mkutano ulifanyika kwenye ukumbi wa shule ya Sekondari Ikungi Mhe Mtaturu alisema kuwa Mbunge huyo amekuwa mfano wa kuigwa kwani amejikita katika shughuli za maendeleo zaidi katika jimbo lake jambo ambalo linaamsha ari kwa wananchi kushiriki shughuli za maendeleo.

Aliwasihi wananchi kwa ujumla kuendelea kumuunga mkono mbunge huyo kwa ushirikiano wake na viongozi wa serikali za mitaa na Madiwani wa Kata zote sambamba na kumuunga mkoano mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kwa weledi na ufanisi wanaoufanya katika uwajibikaji.

Mhe Mtaturu alisema kuwa Jimbo la Singida Magharibi ndilo pekee katika Wilaya ya Ikungi ambalo limeonekana kuwa katika ramani ya uwajibikaji kupitia mbunge wake tofauti kabisa na Jimbo la Singida Mashariki ambalo maendeleo yake yanasuasua kutokana na chuki za kisiasa.

Aliongeza kuwa Mbunge Kingu amekuwa ni kinara wa kusemea hoja na changamoto za wananchi wa Wilaya ya Ikungi kwa ujumla mara kwa mara katika kipindi chote anapokuwa Bungeni nanje ya Bunge nakuongeza kuwa huo ndio uwakilishi unaotakiwa.

Akizungumza kabla ya kuanza kwa uchaguzi wa viongozi wa jumuiya ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Ikungi Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki Mhe Elibariki Kingu alisema kuwa kwa sasa Wilaya ya Ikungi imepata kiongozi imara ambaye anajali maslahi ya wananchi hivyo imani yake maendeleo yatazidi kuimarika kwa wananchi.

Aliwasihi Vijana kushikamana na kuchagua kiongozi bora na si bora kiongozi ili kuendeleza ufanisi wa jumuiya hiyo ambayo ndio muhimili wa Cham Cha Mapinduzi.

Aidha, alisema ataendeleza zaidi ushirikiano baina yake ya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu ili kuwanufaisha wananchi na kuboresha zaidi umoja na mshikamano uliopo pasina kuwabagua wananchi kwa itikadi za Chama, Dini ama Kabila.

MWISHO.

No comments: