Advertisements

Thursday, December 28, 2017

MKE WA BILIONEA MSUYA SASA KULA MWAKA MPYA MAHABUSU

Mke wa marehemu Bilionea Erasto Msuya, Miriam Mrita na mwenzake, wanaokabiliwa na kesi ya mauaji ya dada wa bilionea huyo, Aneth Msuya, bado wanaendelea kukaa mahabusu baada ya upande wa Jamhuri kudai upelelezi haujakamilika.

Kesi hiyo ilitajwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Patrick Mwita, alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuomba mahakama kupanga tarehe nyingine ya kutajwa.

Hakimu alisema kesi hiyo itatajwa Januari 8, 2018 na washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu.Mbali ya Miriam, mshtakiwa mwingine ni mfanyabiashara Revocatus Muyela.

Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuwa Mei 25, 2016 walimuua kwa makusudi dada wa marehemu bilionea Erasto Msuya, Aneth Msuya.

No comments: